LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 27, 2022

PROF. NDALICHAKO: ZAIDI YA TSH.BILIONI 8 ZIMETUMIKA KUWEZESHA VIJANA KUPITIA MRADI WA FEED THE FUTURE TANZANIA

 

IMG_0029

IMG_0040

IMG_0032

IMG_0033


Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako   ameagiza mamlaka za serikali za mtaa kuendelea kuwezesha vijana kupata mikopo pamoja na uwezeshaji wa miundombinu kwa ajili ya watu wenye ulemavu.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Prof.Ndalichako amebainisha hao leo Julai 27,2022 jijini Dodoma  kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  katika ufungaji wa program ya Feed  the Future  Tanzania inua vijana chini ya   ufadhili  wa  shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa[ USAID].

Aidha,Prof.Ndalichako amesema Programu ya The Future imetumia zaidi ya Tsh.Bilioni 8 katika kuwezesha vijana  na kuhimiza USAID kupanua wigo kwa mikoa mingine ili kuwezesha vijana wengi kushiriki kuleta maendeleo hapa nchini.

Katika hatua hatua nyingine Prof.Ndalichako amesema serikali imeanza mchakato wa ujenzi wa vituo vitano   kwa ajili ya kuendeleza vijana.

Mkurugenzi  wa utawala kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI  Victor Kategure amesema Mradi wa Programu ya Feeda the  Future  Tanzania inua vijana umetekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano tangu mwaka 2017 hadi sasa ukilenga vijana wenye umri kuanzia miaka  15 hadi 35.

Mkurugenzi mkuu  shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa [ USAID] nchini Tanzania,Kate Somvongsiri   takriban vijana laki nane [800,000 wanaingia katika nguvu kazi ya Tanzania wakiwa na matarajio madogo sana  au hata bila matarajio ya kupata ajira.

Aidha ,amesema serikali ya Marekani imekuwa ikishirikiana na serikali ya Tanzania katika kuhakikisha vijana wainua uchumi wao ambapo amesema ni muhimu vijana kupewa ujuzi  na ushirikishwaji kwenye sekta ya kilimo ambapo karibu asilimia 67 ya nguvu kazi ya Tanzania  inajishughulisha na kilimo.

Ufungaji wa  Programu ya Feed the Future Tanzania Inua Vijana  umekwenda sambamba na kaulimbiu isemayo “Vijana ni Nguvu Kazi ya Taifa”ambao ulikuwa umejikita zaidi katika mikoa ya Mbeya ,Iringa , na visiwani Zanzibar katika kuwainua vijana kiuchumi kupitia miradi ya kilimo na ufugaji ambapo zaidi ya vijana 43,000 wamepata mafunzo ya ujasiriamali,utayari na nguvu kazi ,uongozi  na stadi za maisha  kwa ajili ya kuishi na kupanga maisha bora.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages