Wajumbe wa Baraza la Utekelezaji la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Newala mkoani Mtwara wakiwa kwenye Kikao cha kujadili na kutoa mapendekezo ya wagombea uongozi nafasi mbalimbali ngazi za Kata, kilichofanyika jana Jumatatu Julai 18, 2022 katika Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya hiyo.
Kutoka kushoto ni Mbunge wa Newala Vijijini Mh. Maimuna Mtanda, Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji wilaya Hawa Mkwamba, Katibu wa UWT wilaya hiyo ya Newala Aminata Mambia na Mbunge wa Newala Mjini Mh. George Mkuchika.
Mh. Mkuchika na Mbunge mwenzake waliingia katika kikao hicho 'kusapoti' kwa kuwa nao walikuwa na kikao chao cha Kamati ya Siasa ya Wilaya toka juzi ambacho kilifanyika pia katika ofisi hiyo ya CCM Wilaya.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇