LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 23, 2022

KATIBU MKUU WIZARA YA MADINI AFUNGUA KIKAO CHA WATAALAMU SEKTA YA MADINI









Katibu Mkuu Wizara ya Madini Adolf Ndunguru amezipongoza Taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Madini kwa ushirikiano waliouonesha katika Mwaka wa Fedha uliopita (2021/22) kwa kufanikisha kufikia malengo ya makusanyo.


Ndunguru ametoa pongezi hizo leo Julai 23, 2022 wakati akifungua kikao cha Wataalamu wa Sekta ya Madini wa Wizara hiyo na Taasisi zilizo chini yake kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara Mtumba jijini Dodoma.


Ndunguru amewataka wataalamu wa Sekta ya Madini kuendeleza ushirikiano katika utendaji kazi wao ili mwisho wa siku waweze kufikia malengo waliyopangiwa na serikali.


Kwa upande wake, Kamishna wa Madini Dkt. Abdulrahman Mwanga amesema kikao hicho kimelenga kujadili mikakati ya kufanya ili kufanikisha kukusanya maduhuli ambayo kwa Mwaka wa Fedha (2022/23) wizara imepangiwa kukusanya kiasi cha Tsh milioni 822,018,203,000.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages