Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amesema katika taarifa kuwa, "vitisho vinaongezeka na gharama ya kutochukua hatua iko wazi," akisema mpango huo wa ulinzi unafaa kuwa tayari ifikapo mwaka 2030.
Umoja huo umesema unahitaji kuwa na uwezo wa kulinda raia wake na kuchangia amani na usalama wa kimataifa kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine. Viongozi wa EU wanatarajiwa kutia saini mpango huo wa usalama, unaojulikana kama dira ya kimkakati, katika mkutano wa kilele utakaofanyika Alhamisi na Ijumaa mjini Brussels.

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇