LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 26, 2022

MWANASHERIA MKUU ASHIRIKI MKUTANO WA SADC KWA NJIA YA MTANDAO

Na Mwandishi Maalum
Mwanasheria Mkuu wa  Mhe. Jaji Dkt Eliezer Feleshi jana (jumanne) ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Wanasheria Wakuu na Mawaziri wa Sheria wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za  Kusini mwa Afrika ( SADC).
 
Pamoja na mambo mengine katika Mkutano huo uliofanyika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa njia ya  mtandao, Wajumbe wa mkutano huo wamepitisha mabadiliko ya Ibara ya 9 ya Mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ( SADC Treaty) kwa kuongeza Bunge la SADC  ili  kuipa mamlaka Jukwaa la Bunge la SADC kuwa Bunge Kamili.

Vile vile  Mkutano  huo pia  umepitisha Mkataba   unaofanya mabadiliko katika Itifaki ya Utalii ( Draft Agreement amending SADC Protocoal on  development of Tourim) na Kanuni za Dhamana ya  usafirishaji wa mizigo katika Kanda ( Revised Regional Customs Transit Gurantee Regulations).

Katika  Mkutano huo,  Mwanasheria Mkuu   aliambatana  na wataalamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ,  Ofisi ya Waziri Mkuu, Afisi ya Rais Zanzibar, Wizara ya Katiba na Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushrikiano wa Kimataifa, Wizara ya  Fedha, Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Nchi wanachama walioshiriki mkutano huo kwa  njia ya mtandao ni  Angola, Botswana, Congo, Eswatini, Lesotho,Mozambique, Madagascar,Nambia, South Afrika, Zambia, Zimbabwe na Tanzania.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa  Wanasheria Wakuu na Mawaziri wa Sheria kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika. (SADC) Mkutano huo umefanyika jana katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Jijini Dodoma

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages