LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 8, 2021

BENKI YA DUNIA YATOA SH. BILIONI 349 KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MAWASILIANO NCHINI+video

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew akizungumza na Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Dkt Tim Kelly kutoka Marekani ambaye yupo nchini na jopo lake kutathmini maandalizi ya uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano nchini. Benki ya Dunia imetoa mkopo wa masharti nafuu sh. bilioni 349 za kugharamia uboreshaji wa miundombinu hiyo.



Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Kundo Mathew akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma Novemba 8, 2021, pamoja na ujumbe kutoka Benki ya Dunia ambao umetua nchini kutathmini maandalizi ya uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano nchini. Benki ya Dunia imetoa mkopo wa masharti nafuu sh. bilioni 349 za kugharamia uboreshaji wa miundombinu hiyo. Kushoto ni Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Dkt Tim Kelly.



Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama, Samson Mwera akizungumza wakati wa mkutano huo kuhusu mikakati iliyowekwa kutekeleza kwa ufanisi uboreshaji huo kufikia Tanzania ya Kidijitali.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Serikali Mtandao, Benadickt Ndomba akielezea jinsi walivyojiandaa kwa ajili ya uboreshaji wa mitandao nchini kwa kutumia fedha hizo.

Naibu Waziri, Kundo na Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Dkt Tim Kelly wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wataalamu wa wizara na maofisa wa Benki ya Dunia.

    Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Prisca Ulomi akiwa na Mwakilishi wa Benki ya Dunia, Dkt Tim Kelly.


PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA


Mdau, nakuomba uendelee kusikiliza kupitia clip hii ya video ujue kilichozungumzwa  na Naibu Waziri Kundo,  viongozi wa taasisi na ofisa wa Benki ya Dunia.....
 

Imeandaliwa na Richard Mwaikenda
 Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages