Katika kikao hicho, Katibu Mkuu wa Posta Afrika, Dkt Moyo amempatia taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Posta Afrika jijini Arusha litakalokuwa la ghorofa 17, kuwa hadi sasa ujenzi wake umefikia ghorofa 12.
Dkt. Moyo atahudhuria kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Posta Duniani kesho Oktoba 9, ambayo kwa hapa nchini yatafanyika kwenye ukumbi wa Jakaya Kikwete Dodoma na mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango.
Waziri Kijaji akizungumza na mgeni wake, Katibu Mkuu wa PAPU, Moyo.
Waziri Kijaji akiongoza mazungumzo na maafisa wa PAPU na wa wizara hiyo ofisini kwake Mtumba.
PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇