LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 13, 2021

MWENYEKITI WA KAMPUNI ZA ASAS ALHAJ FARAJ AHMED ABRI AFARIKI DUNIA LEO, NI BABA YAKE M-NEC SALIM ASAS WA IRINGA

Iringa, leo

Mwenyekiti wa Kampuni za Asas Group, Alhaj Faraj Ahmed Abri ambaye ni Baba mzazi wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Salim Abri Asas amefariki dunia leo Ijumaa Agosti 13 alfajiri, akiwa jijini Dar es Salaam.


Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika familia hiyo, Mzee Abri , maziko yake yatafanyika leo baada ya Swalat Adhuhuri katika Makaburi ya Kisutu Dar es Salaam.


"Hakutakuwa na mikusanyiko kwa tutakaokuwa Iringa, tafadhali tutumie zaidi teknolojia za habari kutoa pole na shughuli nyingine," ilieleza taarifa hiyo.


Mwenyekiti wa CCM, Manispaa ya Iringa Said Rubeya alithibitisha taarifa hiyo na kutoa pole kwa familia, wafanyakazi wa Asas, ndugu jamaa na marafiki.


"Kama tulivyo shauriwa tutumie teknolojia ya habari na mawasiliano kuomboleza, nitoe pole nyingi kwa familia, pole pia kwa M NEC wetu, Salim Asas. Hakika kwa Mwenyezi Mungu ni marejeo," alisema Rubeya.

Alhaj Faraj Ahmed Abri

SORCE: Mwananchi Online

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages