LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 11, 2021

URASIMISHAJI BIASHARA ZA BODABODA/BAJAJI MBIONI KUANZA-MKURABITA


Kaimu Mkurugenzi wa Kurasimisha Ardhi na Biashara wa  Mpango wa Kurasimisha Ardhi na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), Jane Lyimo akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau  wakati wa kuwasilisha  Taarifa ya Tathmini ya Utafiti wa Msingi wa Biashara ya Bodaboda/Bajaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kilichofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu jijini Dodoma leo Agosti 11,2021.

Akizungumza katika kikao hicho, Lyimo amesema kuwa lengo la utafiti huo ni  kuandaa mpango wa kurasimisha shughuli za  waendesha bodaboda na bajaji ili wawe kwenye mfumo rasmi  wa kuaminiwa kukopesheka na taasisi za fedha kuboresha maisha yao kiuchumi.

Lyimo amesema kuwa shughuli za urasimishaji  wa vyombo hivyo, unaakisi dhana ya mpango wa Mkurabita wenye lengo la  kuwawezesha wananchi kurasimisha rasilimali na biashara wanaomiliki na kuzitumia kama nyenzo ya kujiongezea  kipato, mitaji na kupanua wigo wa ushiriki katika uchumi wa kisasa, unaoongozwa na sheria na kanuni za uchumi wa soko la ushindani.

Aidha, Lyimo amesema kuwa utafiti huo ulifanyika jijini Dodoma ni maandalizi ya uzinduzi wa urasimishaji wa shughuli hizo kwa nchi nzima ambapo wataanzia Makao Makuu ya Nchi Dodoma.

Naye, Afisa Urasimishaji na Uendelezaji Biashara wa MKURABITA, Zabron Makoye ameeleza  jinsi utafiti ulivyofanywa na matokeo yake kuwa walianza kwa kukusanya dodoso za waendesha bodaboda/bajaji  zilikusanywa kwa  kwa kutumia simu janja na kwamba dodoso hizo  zilitumika  kupata taarifa za biashara.

Amesema kuwa uchambuzi wake ulilenga kupata taarifa za mahitaji halisi ya biashara hiyo ili kuwezesha timu ya urasimishaji kupanga vizuri mafunzo yaliyolenga kutatua changamoto ambazo wafanyabiashara walengwa  wanakumbana nazo.




Afisa Urasimishaji na Uendelezaji Biashara wa MKURABITA, Zabron Makoye akielezea  jinsi utafiti ulivyofanywa na matokeo yake kuwa walianza kwa kukusanya dodoso za waendesha bodaboda/bajaji  zilikusanywa kwa  kwa kutumia simu janja na kwamba dodoso hizo  zilitumika  kupata taarifa za biashara.
Meneja Urasimashaji Biashara wa MKURABITA,Hancy Kombe akichokoza mada wakati wa kikao hicho. 

Baadhi ya wadau wakiwa katika kikao hicho


Kikao kikendelea

Afisa Mfawidhi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) Dodoma, Ezekiel Emmanuel akichangia mada wakati wa kikao hicho.
Meneja Mauzo wa Kanda wa Benki ya NMB, Ungandeka Mwakatage akielezea kuhusu vigezo vya kukopa fedha kwenye benki hiyo.




Katibu wa Umoja wa Waendesha Bodaboda Mkoa wa Dodma, Remigius Fulgence akielezea namna wanachama wao wanavylaghawiwa na wwatu wanaoingia mikataba ya kuendesha bodaboda ambapo muda ukikaribia wa kumaliza mkataba wanazushiwa jambo linalosababisha kutokabidhiwa bodaboda kama walivyokubaliana awali. Amesema kuwa  urasimishaji unaotarajiwa kufanywa na MKURABITA utakuwa ni ukombozi kwao.

       

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS - IKULU

 

 

 

MPANGO WA KURASIMISHA

RASILIMALI NA BIASHARA ZA WANYONGE TANZANIA

 

MKURABITA

 

TAARIFA YA TATHMINI YA UTAFITI WA MSINGI KWA BIASHARA YA BODA BODA/ BAJAJI KATIKA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA

 

 

 

 

 

AUGUST, 2021


YALIYOMO

 

1.0        Utangulizi 4

1.1        Lengo la Kuanzishwa MKURABITA.. 4

2.0        Majukumu ya wadau wa urasimishaji biashara ya bodaboda. 6

2.1        Halmashauri ya jiji la dodoma. 6

2.2        Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). 6

2.3        Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) 6

2.4 Polisi – Kitengo Cha Usalama Barabarani 7

2. Taasisi za kifedha nI CRDB, NMB NA EQUITY NA AMANA BENKI 7

2.6 Shirika La Taifa La Hifadhi Ya Jamii (NSSF). 7

2.7        Umoja Wa Madereva Pikipiki Dodoma – UMAPIDO.. 8

3.0 Utekelezaji Wa Shughuli Za Urasimishaji Biashara Ya Boda Boda Na Bajaji 8

3.1  Kazi ya Uwandani na Methodolojia. 9

3.2 Lengo La Tathmini Ya Utafiti Wa Msingi Kwa Waendesha Boda Boda 10

4.0 Matokeo Ya Tathmini Ya Utafiti Wa Msingi Kwa Waendesha Boda Boda. 11

4.1 Kubaini umiliki wa boda boda na Bajaji 11

4.2        Kubaini upatikanaji wa Mitaji na Mauzo kwa waendesha Boda/Bajaji 12

4.3        Kubaini usajili wa biashara ya bodaboda/bajaji 13

4.4        Kubaini upatikanaji wa ajira kupitia bodaboda/bajaji 15

4.5        Kubaini upatikanaji wa mikopo ya bodaboda/bajaji 16

4.6        Kubaini upatikanaji na uhitaji wa mafunzo ya urasimishaji 16

 


VIFUPISHO VYA MANENO

BRELA           : Wakala wa Usajili wa Biashara

MKURABITA : Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za     

                             Wanyonge Tanzania

NSSF              : Mfuko ya Hifadhi ya Jamii

TEHAMA        : Teknolojia, Habari na Mawasiliano

TRA                : Mamlaka ya Mapato Tanzania

TIN                  : Nambari ya Mlipa Kodi

TRA                : Mamlaka ya mapato

LATRA               : Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini

UMAPIDO         : Umoja wa Madereva Pikipiki Dodoma

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

1.0       UTANGULIZI

Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA)

Ilianzishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 30 Septemba, 2003 kwa Tamko la Rais wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa. Utekelezaji wa MKURABITA umeanza rasmi Novemba 2004 Tanzania Bara na Zanzibar.Azma ya Serikali ni kuwezesha watanzania wengi kushiriki katika fursa za uchumi kupitia rasilimali na biashara zilizorasimishwa.

 

1.1       Lengo la Kuanzishwa MKURABITA

Lengo la serikali kuanzisha MKURABITA ni kuwawezesha wananchi wanaomiliki rasilimali na kuendesha biashara nje ya mfumo rasmi waweze kuzirasimisha na kuzitumia kupata mitaji kwa ajili ya kushiriki katika uchumi wa kisasa unaondeshwa kwa mujibu wa sheria.

 

 

 

 

M

KURABITA kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za mitaa inatekeleza dhana ya Uanzishwaji wa Kituo Jumuishi cha Urasimishaji,uwekezaji na Uendelezaji Biashara katika Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Mantiki ya kuanzishwa MKURABITA imejengwa katika msingi wa umuhimu wa kuwawezesha wamiliki wa rasilimali na biashara nje ya mfumo rasmi kuingia katika mfumo rasmi. Kuingia kwao katika mfumo rasmi kutawawezesha kutumia rasilimali na biashara zilizorasimishwa kupata na kukuza mitaji ya shughuli zao za kiuchumi. Hali hii itachangia kupunguza umasikini wa kipato katika kaya, na hatimaye kuchangia kuinua uchumi wa taifa kwa ujumla.

 

Katika kutekeleza maelekezo ya kurasimisha shughuli za Bodaboda yaliyotolewa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Deogratius John Ndejembi alipofanya ziara MKURABITA Desemba 2020, Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA imeweza kukutana na mdau mmoja mmoja wa Usimamizi wa shughuli za usafiri wa Bodaboda na Bajaji nchini. Wadau hao ni pamoja na Polisi, LATRA, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, UMAPIDO, NMB, CRDB, Equity na Amana Benk. Mazungumzo na mdau mmoja mmoja yamewezesha maandalizi ya rasimu ya Mpango wa Kurasimisha biashara ya pikipiki maarufu kama bodaboda katika jiji la Dodoma.

Lengo la Serikali ni kuwawezesha wafanyabiashara wa Boda boda na Bajaji kuendesha shughuli zao kwa mujibu wa Sheria na hivyo kuwezesha kuchangia uwepo wa ajira na pato la taifa kwa ujumla wake. Kupitia biashara rasmi ya Bodaboda na Bajaji  wamiliki watakuwa na uwezo wa kupata mtaji na hivyo kufanya biashara endelevu na himilivu. Mpango wa kurasimisha shughuli za Boda boda na Bajaji umezingatia majukumu ya msingi ya kila mdau kama yalivyoainishwa:

 

2.0       MAJUKUMU YA WADAU WA URASIMISHAJI BIASHARA YA BODABODA

Wadau katika Mpango huu ni wote wanaojihusisha na shughuli za urasimishaji biashara ya bodaboda ikiwemo usajili, leseni, Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi na uzingativu wa usalama barabarani. Aidha, kwa kuwa lengo kuu ni kuwezesha wamiliki kiuchumi, Taasisi za fedha ni sehemu ya wadau muhimu. Yafuatayo ni majukumu ya msingi ya wadau wa urasimishaji biashara Bodaboda na Bajaji:-

2.1       HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA

Pamoja na mambo mengine majukumu mahsusi katika Halmashauri ya Jiji huu ni:- Kutoa leseni kwa pikipiki za magurudumu miwili na matatu kwa kuzingatia kanuni za leseni za usafirishaji zilizowekwa na LATRA; kufanya utambuzi na usajili wa vituo vya Bodaboda na Bajaji na katunza na kuhuisha orodha ya bodaboda/bajaji zilizosajiliwa :

 

Timu ya Urasimishaji biashara ya boda boda  fursa ya kuonana na  Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma, Mkuu wa wilaya ya Dodoma na baadae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma  kwa dhumuni la kutambulisha timu ya wataalam kutoka MKURABITA kuwa Urasimishaji Biashara  ya boda boda na Bajaji utafanyika katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Timu ilikuwa na Afisa kutoka MKURABITA, Viongozi wa Boda boda na Bajaji, Afisa Biashara na Maafisa Watendaji wa Mitaa na Kata, na Wataalam wengine ngazi ya Kata na Mitaa ndiyo walikuwa wakusanya Taarifa za waendesha boda boda na Bajaji pia uhakiki wa vituo ulifanyika katika maeneo yaliyachagulikuwa kukusanya Taarifa.

2.2       MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA)

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wanalo jukumu kubwa la kukusanya na kusimamia mapato nchini. Majukumu mahsusi katika mpango huu ni:- Usajili wa chombo cha moto na Usajili wa Namba ya Utambulisho wa Mlipa Kodi (TIN), Ukusanyaji wa kodi ya Serikali.

2.3     MAMLAKA YA UDHIBITI WA USAFIRI ARDHINI (LATRA) – MKOA WA DODOMA

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini wanalo jukumu kubwa la kudhibiti usafiri wa barabara. Katika Mpango huu majukumu mahsusi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini ni pamoja na:-Kutoa leseni za kuendesha biashara ya Bodaboda na Bajaji baada ya mmiliki kusajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania, Kutathmini ubora wa vituo na kusajili vituo vya kupakia abiria wa Bodaboda na Bajaji kwa kushirikiana na Halmashauri ya Jiji la Dodoma; Kuweka na kusimamia viwango, masharti na gharama za huduma kwa mujibu wa sheria na Kukuza ushirikiano na taasisi zingine za Serikali

2.4 POLISI – KITENGO CHA USALAMA BARABARANI MKOA WA DODOMA, (MKAGUZI WA POLISI MKOA)

Kitengo cha Usalama Barabarani kina wajibu wa kusimamia na kuhakikisha usalama wa mali na watumiaji barabara. Majukumu mahsusi katika Mpango huu ni:- Kusimamia usajili wa vyombo vya moto na kuvifanyia ukaguzi wa ubora ikiwemo usalama barabarani; Kutoa leseni za udereva kwa madereva wa vyombo vya moto ambao wamefuzu mafunzo na kuwa na Register (rejesta) kanzi data  ya Vituo vya Bodaboda na Bajaji ambavyo vimesajiliwa na vinaendeshwa kwa kufuata taratibu na kanuni zilizowekwa;

 

2.5  TAASISI ZA KIFEDHA NI CRDB, NMB NA EQUITY NA AMANA BENKI

Taasisi za fedha zina jukumu la msingi la kupokea na kutoa fedha kwa wateja wake. Jukumu mahsusi la mabenki haya ambayo ni wadau wa Mpango wa urasimishaji biashara ya Waendesha Boda boda na Bajaji ni:- Kutoa mikopo ya pikipiki na bajaji kwa walengwa wa Mpango huu;Kuhamasisha wamiliki wa bodaboda kufungua akaunti za benki na kukopa fedha kwa ajili ya kuendesha biashara zao; Kuwezesha na kutoa mafunzo kwa waendesha Bodaboda na Bajaji juu ya namna bora ya usimamizi wa mikopo na kuratibu na kusimamia maendeleo ya biashara zilizotokana na mikopo ya benki.

2.6 SHIRIKA LA TAIFA LA HIFADHI YA JAMII (NSSF)

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) katika Mpango huu inahusika kusajili wananchama ambao ndiyo waendesha Boda Boda na Bajaji ili waweze kujiwekea akiba uzeeni ambapo Jukumu la Mfuko huu ni kutoa elimu kwa waendesha Boda boda na Bajaji ili waweze kujiunga na kuchangia michango yao ya kila mwezi kwa mujibu wa sherie ya Mfuko huu.

 

2.7       UMOJA WA MADEREVA PIKIPIKI DODOMA – UMAPIDO

UMAPIDO ni umoja wa hiari ulioundwa na kusajiliwa kisheria kwa madhumuni ya kuhudumia madereva wa pikipiki za magurudumu miwili na matatu. Aidha UMAPIDO una muundo wa uongozi unaoongozwa na Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina na Kamati nne (4) ambazo ni; Kamati ya Ulinzi, Maafa, Fedha na Nidhamu: Majukumu mahsusi ya UMAPIDO katika Mpango huu ni:- Kusajili taarifa za madereva pikipiki pamoja na vituo. Taarifa hizi (kanzidata) zinapatikana kwa kushirikiana na jeshi la Polisi na LATRA; Kutambua wamiliki na waajiriwa wa pikipiki;Kupendekeza kwa LATRA usajili wa vituo vipya au kufuta kituo vya zamani kama usalama wake ni wa mashaka na Umoja unadhamini wanachama wake wanapotaka kukopa katika vyombo vya fedha.

3.0 UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA URASIMISHAJI BIASHARA YA BODA BODA NA BAJAJI

Shughuli za urasimishaji biashara ya waendesha Boda boda na Bajaji zilizopangwa kutekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, zinaakisi dhana ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA), wenye lengo la kuwezesha wananchi kurasimisha rasilimali na Biashara wanazomiliki na kuzitumia kama nyenzo ya kujiongezea kipato, mitaji na kupanua wigo wa ushiriki katika uchumi wa kisasa, unaoongozwa na sheria na kanuni za uchumi wa soko la ushindani.

 

Aidha, MKURABITA kufuatia makubaliano na kikao cha kwanza cha wadau kilichofanyika Takwimu House Dodoma mnamo tarehe 26 May,2021 ilikubaliwa kuwa MKURABITA afanye Tathmini ya Utafiti wa Msingi kwa waendesha Boda boda na Bajaji, kuhakiki vituo vilivyosajili na kuanda na kuhuisha kanzi data ya waendesha Boda boda na Bajaji katika Halmashauri ya jiji la Dodoma. Zoezi la Urasimishaji Biashara ya Boda boda na Bajaji lilianza kwa kufanya tathmini ya utafiti wa msingi kwa waendesha Boda boda na Bajaji wa jiji la Dodoma ilianza 23/06/2021 kwa kukusanya na kufanya upembuzi wa awali na mnamo tarehe 10 Julai, 2021ilihitimisha zoezi kwa kukusanya taarifa za waendesha boda boda na Bajaji 2,077 kilelezo Na.1 Kimeabatanishwa Kanzi data ya biashara ya waendesha Boda Boda na Bajaji zilizokusanywa (baseline).

3.1 KAZI YA UWANDANI NA METHODOLOJIA ILIYOTUMIKA  

Kazi zilizopangwa ilikuwa ni Kukusanya takwimu za biashara ya waendesha Boda boda na Bajaji kwa ajili ya Tathmini ya Utafiti wa Msingi msingi (Business baseline survey) na kuendesha mafunzo ya urasimishaji biashara ya Boda boda na Bajaji.

Kazi ilianza uwandani kwa lengo la kukusanya taarifa za wafanyabiashara ya Boda boda na Bajaji  2,500  tarehe 23 Juni, 2021 hadi 10 Julai, 2021 ilifanyika kwa kukusanya Taarifa za waendesha Boda boda na Bajaji kupitia dodoso.Takwimu za waendesha Boda boda na Bajaji zilikusanywa kwa mfumo wa Tehama ambapo mdodosaji aliweza kuandika taarifa za biashara ya boda boda kwa kutumia simu ya kiganjani “Smart phone”, iliyowekewa Mfumo wa kukusanya taarifa (kobocollect program) na dodoso lilitumika kupata taarifa za biashara.

Picha Na.1 Picha ikionesha Mafunzo ya Wakusanya Takwimu za Boda Boda/Bajaji

 

Hivyo, mbinu na njia zilizotumika kukusanya taarifa za biashara ya Boda boda ilikuwa ni dodoso lililohifadhiwa kwenye simu, Takwimu za biashara ya Boda boda na Bajaji zilikusanywa kwa ajili ya kubaini mahitaji na changamoto katika kurasimisha na kuendesha biashara zao ambapo mhojiwa aliweza kutoa taarifa zake kwa njia ya majadiliano na mhojaji aliweza kujaza dodoso hilo na kutuma moja kwa moja kwenye server kuu, iliyokuwa inasimamiwa na Ofisi ya MKURABITA na baada ya taarifa kukusanywa zilichambuliwa kupitia mfumo wa “Excel Analyser”; baada ya uchambuzi, taarifa ya matokeo imeandikwa kwa kuzingatia malengo mahsusi ya tathmini.

 

Picha Na 2: Mafunzo ya Mfumo kwa Wakusanya Taarifa za Boda boda na Bajaji

Uchambuzi wake ulilenga kupata taarifa za mahitaji halisi ya biashara ya boda boda na Bajaji ili kuiwezesha timu ya urasimishaji kupanga vizuri mafunzo yaliyolenga kutatua changamoto ambazo wafanyabiashara walengwa wamekuwa wakikumbana nazo katika uendeshaji wa biashara ya Boda boda na Bajaji.

3.2 LENGO LA TATHMINI YA UTAFITI WA MSINGI KWA WAENDESHA BODA BODA NA BAJAJI JIJI LA DODOMA

Tathmini ya utafiti wa msingi kwa wafanyabiashara wa Boda boda na Bajaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma hutumika kubainisha aina ya mafunzo yanayotakiwa kutolewa na Namba ya Utambulisho wa mlipa kodi, usajili wa biashara ya Boda boda na Bajaji, leseni za udereva, leseni ya usafirishaji Piki Piki na Bajaji.

Aidha, zoezi la tathmini ya msingi ililenga kufanyika sambamba na usajili wa biashara ya Boda boda na bajaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma. Malengo mahsusi ya tathmini yalikuwa Kama ifuatavyo:-

        i.          Kubaini umiliki wa biashara za Boda boda na Bajaji

      ii.          Kubaini waendesha boda boda na bajaji

     iii.          Kubaini upatikanaji wa mitaji na mauzo;

     iv.          Kubaini usajili wa biashara ya boda boda na Bajaji;

      v.          Kubaini upatikanaji wa ajira kupitia biashara ya Boda boda na Bajaji;

     vi.          Kubaini upatikanaji wa mikopo kwa wafanyabiashara wa Boda bodaa;

    vii.          Kuwezesha biashara Boda boda kuwa na mahusiano na Taasisi za kifedha ili kupata huduma zitolewazo na Taasisi hizo.

  viii.          Kubaini upatikanaji na uhitaji wa mafunzo ya urasimishaji biashara ya Boda boda

 

4.0 MATOKEO YA TATHMINI YA UTAFITI WA MSINGI KWA WAENDESHA BODA BODA NA BAJAJI KATIKA HALMASHAURI YA JIJI LA DODOMA

Ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa za biashara ya waendesha Boda boda na Bajaji 2,077 ulifanyika na kufanikiwa kufanya uchambuzi na matokeo ya uchambuzi wa taarifa umeonyesha; Matokeo kwa kila lengo mahsusi yameelezwa katika kipengele Na. 4.1 hadi 4.6 Kama ifuatavyo:

4.1 Kubaini umiliki wa Boda boda na Bajaji

Kubaini sifa muhimu za wamiliki wa biashara kama jinsia, umri, umiliki ni muhimu katika kuainisha mahitaji halisi ya watumiaji wa boda/Bajaji ili kuwezesha kuandaaji wa mipango ya maendeleo. Matokeo kwa Muhtasari ni kama yanaovyoonekana kwenye kielelezo Na. 1 na maelezo ya kina yanachambuliwa:-

a)         Utumiaji wa boda boda na bajaji; eneo hili lilibainishwa ili kupata hali kiwango cha watumiaji wa bodaboda na bajaji. Matokeo yanaonesha, kati ya watumiaji 2,077 waliofikiwa, asilimia 87 wanatumia bodaboda ikilinganoshwa na asilimia  ya biashara 13 bajaji, hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau kutoa kipaumbele kwa kundi hili kubwa.

b)      Aina ya Umiliki: Kubaini umiliki ni eneo muhimu ili kubaini aina ya umiliki wa Boda boda/bajajiMatokeo yanaonesha, kati ya watumiaji 2,077, asilimia 61 wanamiliki kwa mkataba ikilinganishwa na asilimia 39 wanaomiliki wenyewe, hivyo serikali kwa kushirikiana na Taasisi za fedha ili kuongeza kasi ya umiliki binafsi wa Boda boda/bajaji kwa kuwawezesha ili kumpa tija mtumiaji.

c)      Jinsia; uchambuzi wa wanawake na wanaume ni kiashiria muhimu katika kubaini mahitaji ya kijinsi kwa waendesha Boda boda na bajaji. Matokeo yanaonesha kati ya watumiaji 2077, Wanawake ni asilimia 1 ikilinganishwa na wanaume asilimia 99. Hali hii inaonesha wanaume ndiyo watumiaji zaidi wa Bodaboda/bajaji, hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo kuongeza kasi ya uhamasishaji kwa wanawake kushiriki na kutumia Bodaboda/bajaji kibiashara.

d)         Umri; Uchambuzi wa umri ni kiashiria muhimu katika kubaini mahitaji ya kwa kuzingatia umri wa watumiaji Bodaboda na bajaji. Matokeo yanaonesha kati ya watumiaji 2, 077, asilimia 84 wana umri kati ya miaka 18-34 ikifuatiwa na asilimia 13 wenye miaka kati 36-44. Hali hii inaonesha uandaaji na utekelezaji wa mipango ya maendeleo utoe kipaumbele hasa kundi la vijana.

e)         Elimu: Uchambuzi wa elimu umefanyika ili kubaini viwango vya uelewa ili kusaidia wakati wa uandaaji mpango wa mafunzo. Matokeo yanaonesha kati ya watumiaji 2,077, asilimia 46 wana elimu ya msingi ikifuatiwa na asilimia 40 wenye elimu ya sekondari. Hali hii inaonesha uandaaji na utekelezaji wa mipango ya maendeleo lizingatie elimu za wamiliki hasa msingi na sekondari.

4.2       Kubaini upatikanaji wa Mitaji na Mauzo kwa waendesha Boda/Bajaji

Upatikanaji wa mitaji na mauzo ni eneo muhimu ili kubaini vyanzo halisi vya mitaji ya waendesha bodboda/bajaji. Matokeo kwa Muhtasari ni kama yanaovyoonekana kwenye kielelezo Na. 2 na maelezo ya kina yanachambuliwa baada ya kielelezo

 

a)         Chanzo cha mtaji: chanzo cha Mtaji ni kiashiria muhimu katika kubaini chanzo cha mapato kwa waendesha boda/bajajiMatokeo yanaonesha, kati ya watumiaji 2,077, asilimia 45 yanatokana na pesa binafsi ikifuatiwa na asilimia 43 inatokanan na mali ya kuazima. Pia, ni asilimia 5 tu ya mitaji inatokana na taasisi za fedha. Hali hii inaonesha, juhudi zinahitajiika kati ya serikali na taasisi za fedha ili kuongeza kasi ya upatikanaji wa mitaji kupitia  mikopo kwa waendesha boda/bajaji. Pia matokeo yanaonesha waendesha boda wana mitaji kati ya chii ya TZS 100,000(asilimia 40) na kati ya 100,000-500,000(asilimia 40) ikifuatiwa na asilimia 17 wenye mitaji zaidi ya TZS 1,000,000

b)         Utunzaji kumbukumbu: Utunzaji kumbukumbu ni muhimu ili kupata taarifa sahihi za mapato na matumizi. Matokeo yanaonesha asilimia 52 ya waendesha boda/bajaji wanatunza kumbukumbu ikilinganishwa na asilimia 48 wasiotunza kumbukumbu.

c)          Mapato: Kiwango cha mauzo ni eneo muhimu ili kubaini ukubwa wa shughuli na ukuaji wake. Matokeo yanaonesha waendesha boda/bajaji wanapata kwa siku wastani wa mauzo ya kati TZS 10,000-50,000 ikifuatiwa na asilimia 45 wanaopata chini ya TZS 10,000.

4.3       Kubaini usajili wa biashara ya bodaboda/bajaji

Usajili wa bajaji na bodaboda ni takwa la kisheria linalosimamiwa na Mamlaka ya Uthibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA). Uchambuzi umezingatia, Usajili wa chombo, Leseni, Vituo, Bima, Matokeo kwa Muhtasari ni kama yanaovyoonekana kwenye kielelezo Na. 3 na maelezo ya kina yanachambuliwa baada ya kielelezo.

a)         Usajili wa kituo; Uchambuzi wa usajili wa vituo vya bajaji/bodaboda ni muhimu ili kupata taarifa za msingi za watumiaji wa bodaboda/bajaji. Matokeo yanaonesha kati ya wamiliki 2,077, asilimia 64 wako katika vituo vilivyosajiliwa kisheria ikilinganishwa na asilimia 36 hawako katika vituo vilivyosajiliwa kiasheria. Hivyo Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa usafiri wa boda/bajaji kuongeza juhudi ya kuhamasisha usajili wa vituo hivyo.

 

b)          Usajili LATRA; Uchambuzi wa usajili wa boda/bajaji ni matakwa ya kisheria chini ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Ardhini (LATRA).  Matokeo yanaonesha kati ya wamiliki 2,077, asilimia 83 wamesajiliwa LATRA ikilinganishwa na asilimia 17 wasio usajiliwa. Hivyo Halmashauri imekasimiwa madaraka kwa kushirikiana na wadau wa usafiri wa boda/bajaji kuongeza juhudi za uhamasishaji usajili wa matumizi  ya vyombo hivyo.

 

c)          Usajili wa Leseni ya Udereva; Uchambuzi wa usajili wa leseni za boda/bajaji ni hitaji la kisheria kwa watumiaji wote kuwa na leseni ya utumiaji wa boda/bajaji.  Matokeo yanaonesha kati ya wamiliki 2,077, asilimia 76 wana leseni za udereva ikilinganishwa na asilimia 23 wasio leseni. Hivyo Halmashauri kwa kushirikiana na wadau kuongeza uhamasishaji kwa watumiaji wa boda/bajaji kuwa na leseni sahihi za  udereva.

 

d)         Usajili wa BIMA; Uchambuzi wa usajili wa leseni za boda/bajaji ni hitaji la kisheria kwa watumiji wote kuwa na Bima ya chombo husika.  Matokeo yanaonesha kati ya wamiliki 2,077, asilimia 84 wana Bima za bodaboda/bajaji ikilinganishwa na asilimia 16 wasio na bima. Hivyo Jiji kwa kushirikiana na wadau wa usafiri wa boda/bajaji kuongeza uhamasishaji kwa watumiaji wa boda/bajaji kuwa na leseni za udereva.

 

4.4 Kubaini upatikanaji wa ajira kupitia bodaboda/bajaji

Upatikana wa ajira ni manufaa kwa mtumiaji na faida kwa ujumla. Uchambuzi umezingatia umiliki wa chombo, ajira, mikataba ya ajira na kujilipa mshahara. Matokeo kwa Muhtasari ni kama yanaovyoonekana kwenye kielelezo Na. 4 na maelezo ya kina yanachambuliwa baada ya kielelezo

 

a)         Wamiliki wa bajaji/boda: Matokeo yanaonesha asilimia 74 ya wamiliki wa bajaji ni wanaume ikilinganishwa na asilimia 24 ambao ni wanawake. Pia, asilimia 2 zinamilikiwa na makampuni kama ubber na bolt.

b)         Mikataba ya ajira: Matokeo yanaonesha asilimia 70 ya watumiaji waliokodishwa wana mikataba ya ajira ikilinganishwa na asilia 30 wasio na mikataba. Matokeo pia, yanaonesha sababu za kutowapa mikataba ni kiutokana na kufanya kazi kama ndugu (asilimia 35) ikifuatiwa na sababu ya kutojua umuhimu wa mkataba (asilimia 30).

c)          Kujilipa mshahara; Matokeo yanaonesha asilimia 77 ya watumiaji wanajilipa mshahara ikilinganishwa na asilimia 23 wasiojilipa.

 

4.5 Kubaini upatikanaji wa mikopo ya bodaboda/bajaji

Upatikana wa mikopo ni fursa za kifedha wanazozipata watumiaji wa bajaji ili kuongeza mtaji. Uchambuzi umezingatia, umiliki wa akaunti na upatikanaji wa Mkopo. Matokeo kwa Muhtasari ni kama yanaovyoonekana kwenye kielelezo Na. 5 na maelezo ya kina yanachambuliwa baada ya kielelezo.

a)          Akaunti za benki (A/C); Matokeo yanaonesha, kati ya wamiliki 2,077, asilimia 25 wana akaunti za benki ikilinganishwa na asilimia 75 wasio na akaunti za benki.

b)         Uombaji mkopo; Matokeo yanaonesha asilimia 18 ya watumiaji wameomba mkopo katika Taasisi za fedha ikilinganishwa na asilimia 82 hawajawahi kuiomba mkopo.

c)          Kupata Mkopo; Matokeo yanaonesha asilimia 78 ya watumiaji waliomba mkopo ndiyo waliopata ikilinganisjhwa na ikilinganishwa na asilimia 25 hawakupata.

d)          Kiasi cha Mkopo; Matokeo yanaonesha asilimia 54 walipata kati ya TZS 500,000-3,000,000 ikifuatiwa na asilimia 39 waliopata chini ya TZS 500,000.

4.6     Kubaini upatikanaji na uhitaji wa mafunzo ya urasimishaji

Upatikana mafunzo kwa waendesha boda/bajaji ni eneo muhimu ili kuongeza ujuzi katika kutekeleza shughuli zao. Matokeo katika kielelezo Na.6 yanaonesha asilimia 87 ya watumiaji wa boda/bajaji wanahitaji mafunzo. Matokeo pia yanaonesha mada zinazopendekezwa ni pamoja na Usajili wa biashara zao (asilimia 53) ikifuatiwa na upatikanaji wa mikopo (asilimia 53) pamoja na utunzaji kumbukumbu (asilimia 53)

 

Hatua za utekelezaji wa zoezi la urasimishaji waendesha Boda boda na Bajaji Dodoma Jiji

Na.

Shughuli

Idadi ya siku

Wahusika

1

Kikao na Wadau Kujadili Rasmu ya Mpango wa urasimishaji biashara boda boda

1

LGA, Wadau na MKURABITA

2

Kujenga Uelewa Kwa LGAs, WEO, MEO na Viongozi wa Boda boda

1

LGA, Wadau na MKURABITA

3

Kukusanya Taarifa za Waendesha Boda boda na kuhakiki vituo vilivyosajiliwa

10

MKURABITA,WEO,MEO,CDO

4

Kuchambua Taarifa zilizokusanywa za waendesha Boda Boda na Bajaji

2

BFDO,RMO, AA,

6

Mpango wa Mafunzo endelevu kwa biashara ya Waendesha  Boda Boda na Bajaji

2

MKURABITA na Wadau

7

Kikao cha wadau kuwasilisha Tathimini ya Matokea ya Utafiti wa Msingi  na maandalizi ya Mafunzo

1

LGA, Wadau na MKURABITA

8

Mafunzo ya Urasimishaji Biashara ya Boda boda/Bajaji

Siku 1 x makundi 6

LGA, Wadau na MKURABITA

9

Usajili wa Biashara ya Boda boda na Bajaji

5

LGA, Wadau na MKURABITA

10

Uwezeshaji wa Boda boda na Bajaji

3

LGA, Wadau na MKURABITA

 

 

 

 

 

 

RATIBA YA KIKAO CHA WADAU WA URASIMISHAJI NA UWEZESHAJI BIASHARA YA BODA BODA NA BAJAJI – DODOMA JIJI, 11/08/2021

Muda

Shughuli

Mahali

Mhusika

11 August. 2021

Kuwasili kwenye ukumbi

Takwimu House

wote

 

04:00 – 05:00

·      Ufunguzi wa kikao

·      Kuwasili na Utambulisho

·      Kusaini Mahudhurio

·      Kupokea Taarifa ya utafiti wa Msingi kwa waendesha Boda boda/Bajaji

Takwimu House

 

 

Maafisa Kutoka MKURABITA

05:00 -05:10

 

 

 

05:10 – 07:00

·         Kujadili Taarifa kwa ufupi

·      Mpango wa utoaji Mafunzo

·      Mpango wa usajili na uwezeshaji wa Biashara ya Boda boda

·      Mpango wa mafunzo endelevu biashara ya Boda boda

·      Ufuatiliaji wa wanufaika wa Biashara ya Boda boda

·      Kufunga kikao

Takwimu House

LATRA, Afisa biashara, TRA,NSSF,NMB,CRDB,Amana, Equity, Polisi usalama barabarani,Umapindo

07:00 – 08:00

Mapumziko ya Chakula & kufunga

Dodoma

Wote

 

 

 

 

 

 

 


Imeandaliwa na Richard Mwaikenda
Mhariri Blog ya Taifa ya CCM
0754264204
 

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages