LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 26, 2021

MAKAMU WA RAIS DKT MPANGO ATEMBELEA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA CHUJIO LA MAJI MKOANI MTWARA

 Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango ametembelea na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa chujio la maji Mangamba unaogharimu shilingi bilioni 2.3, unaotarajiwa kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama mkoani Mtwara.


Makamu wa Rais Dkt Mpango amemtaka Waziri wa Maji Jumaa Aweso kusimamia na kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha mradi kwa wakati ili kuondoa kero zilizopo na kuwapa wananchi maji safi na salama huku akisisitiza kutumia malighafi za ndani zinazokidhi mahitaji na zinazofikia viwango badala ya kuagiza nje ya nchi malighafi ambazo zinaweza kupatikana hapa nchini

Waziri wa Maji Jumaa Aweso amemhakikishia Makamu wa Rais kukamilisha mradi kwa wakati huku akieleza kuwa kwa sasa wizara inawajengea uwezo wataalamu wa ndani ili watumike kujenga miradi ya maji badala ya kuendelea kutegemea wataalamu kutoka nje ya nchi

Makamu wa Rais pia ameitaka Wizara ya Maji kuwa na mpango maalum wa makusudi kusomesha wataalamu wa maji ili kuhakikisha Taifa linakuwa na wataalamu wa kutosha kuhudumu katika sekta ya Maji nchini.




No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages