LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 15, 2021

ALIYEWAHI KUWA WAZIRI NA KIONGOZI WA NGAZI ZA JUU CCM DK. MOHAMMED SEIF KHATIB AMEFARIKI DUNIA, LEO

Dk. Mohammed Seif Kahatib


Na CCM Blog, Zanzibar

Mwanasiasa nguli wa siku nyingi Dk. Muhammed Seif Khatib amefariki Dunia, leo asubuhi katika Hospitali ya Arhama Unguja mjini Zanzibar. Emmanuel Mohamed mtoto wa Khatib, amethibitisha.


Amesema, msiba upo nyumbani kwa marehemu eneo la Magomeni Zanzibar na mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho saa nne asubuhi.


Wakati wa uhai wake Khatibu aliyezaliwa Januari 10, 1951,  amewahi kuhudumu katika nafasi mbalimbali katika Chama Cha Mapinduzi na Serikalini, ikiwemo kuwa  Mbunge wa Jimbo la Uzini  Zanzibar kwa tiketi ya CCM mwaka 1995 na pia amewahi kuwa Waziri katika wizara mbalimbali.


Khatibu atakumbukwa kwa kuwa miongoni mwa waasisi wa kwanza wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) ambapo  kati ya mwaka 1978 hadi 1983 alikuwa Mwenyekiti wa UVCCM  na kati ya mwaka  1978 na 2002 Khatibu alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Pia amewahi kuwa Katibu wa NEC, Oganaizesheni Makao Makuu ya CCM.


Kabla ya kuwa mjumbe wa NEC alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu  anayeshughulikia masuala ya Habari, na baadaye January 4, 2006  aliteuliwa kuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo   na  February 12, 2008 akateuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia masuala ya Muungano.


Msimamizi Mkuu wa Blog ya Taifa ya CCM, Bashir Nkoromo na Waendeshaji wote wa Blog hii tunatoa pole za dhati kwa Ndugu, Jamaa, Marafiki na wote walioguswa kwa namna moja au nyingine na msiba huu. 

Ina Lilah Waina Ilayh Rajiuun.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages