LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 14, 2021

SERIKALI YATANGAZA KUJENGA KIWANDA CHA SIMU JANJA MWANZA

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt Faustine Ndugulile,akizungumza wakati wa kikao kazi na wenyeviti wa bodi na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma Januari 14, 2021. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA



Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano na  Teknolojia ya Habari , Dkt Zainab Chaula,akifafanua jambo  alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari baada  kikao kazi na wenyeviti wa bodi na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara hiyo kilichofanyika jijini Dodoma. 
Mtendaji Mkuu   wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote, UCSAF, Justina Mashiba, akizungumza kwenye kikao kazi na wenyeviti wa bodi na wakuu wa taasisi zilizochini ya Wizara hiyo kilichofanyika  jijini Dodoma.
Baadhi ya viongozi wa taasisi sita zilizo chini ya wizara hiyo, wakiwa makini kusikiliza maagizo ya uboreshaji kazi kutoka kwa Waziri Ndugulile.
Waziri Ndugulile akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho.
Baadhi ya viongozi wa taasisi sita zilizo chini ya wizara hiyo, wakiwa makini kusikiliza maagizo ya uboreshaji kazi kutoka kwa Waziri Ndugulile.

Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dkt. Jim Yonazi akitoa neno la shukrani wakati wa kuhitimisha kikao hicho kilichofanyika Kituo cha Mikutano cha Dodoma.


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Simu la TTCL, Waziri Kindamba akielezea jinsi walivyojidhatiti  kuboresha huduma za shirika hilo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, TCRA, akielezea mafanikio ya kikao kazi hicho na jinsi walivyojipanga kutekeleza maagizo ya waziri pamoja na utekelezaji wa ilani ya chama tawala kuhusu kuinua  na kuboresha sekta ya mawasiliano nchini.



Na Richard Mwaikenda, Dodoma

SERIKALI imeazimia kujenga kiwanda cha kutengeneza simu janja mkoani Mwanza ili kurahisisha  mawasiliano nchini kwa gharama nafuu.

 

Mpango huo umetangazwa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akitoa ufafanuzi kwa wanahabari kuhusu yaliyojiri kwenye  kikao kazi  na viongozi wa taasisi sita zilizochini ya wizara hiyo, jijini Dodoma leo Januari 14, 2021.

 

“Sisi katika wizara mpya hatuwezi kusubiri kutumwa  kazi, tumesoma ilani ya chama imesema tuongeze wigo wa mawasiliano , tuongeze matumizi ya intaneti , hatuwezi kufanikiwa ikiwa wananchi watashindwa kununua  simu janja na kompyuta mpakato, na hili tumeliona na serikali hivi sasa imeanza mchakato wa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza simu janja mkoani Mwanza ili wananchi wapate simu kwa gharama nafuu,” amesema Dkt Ndugulile..

 

Ametoa rai kwa wafanyabiashara wenye nia ya kutaka kuwekeza katika sekta ya mawasiliano waende Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya habari watapewa ushirikiano wa asilimia 100 kuhakikisha zinatengenezwa bidhaa za Tehama ambazo zinaweza kutumika ndani ya nchi ili wananchi wengi wazipate kwa gharama nafuu.

 

Dkt. Ndugulile amesema hivi sasa Serikali inauhitaji mkubwa wa kukuza sekta ya mawasiliano katika maeneo yote, hivyo wabunifu na wawekezaji wenye uwezo wa kuwekeza katika sekta ya mawasiliano wanakaribishwa ili nchi ijenge uwezo binafsi wa kimtandao (TEHAMA) katika kuendesha shughuli zake.

Amesema kuwa malengo ni asilimia 70 ya huduma zinazotolewa na Serikali ziwe zinatumia Tehama kupunguza urasimu ambapo mwananchi badala ya kufuata huduma katika ofisi za serikali, atumie Tehama kulipia kodi kwa kutumia simu janja,  mwanafunzi angalie matokeo yake kwenye mtandao, mkulima aulizie au kununua mbegu kwenye mtandao.

 

Katika  mkutano huo na wanahabari, Waziri amezungumza mengi kuhusu umuhimu wa matumizi Tehama katika karne hii, hivyo nakusihi endelea kumsikiliza Dkt. Ndugulile kupitia kwenye clip hii ya video….


IMEANDALIWA NA; 
 RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM 
0754264203

1 comment:

  1. Ni hatua njema sana na ya kupigiwa upatu. Tunakwenda kupata mawasiliano bora na uhakika. Suala la gharama za INTERNET bado linaumiza mno.

    ReplyDelete

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages