LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 20, 2021

NAIBU WAZIRI WA MAJI MAHUNDI AIKUMBUSHA BODI, BARAZA LA DUWASA MAJUKUMU YAO+VIDEO



Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi akizindua rasmi Baraza la Sita la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Dodoma (Duwasa) jijini Dodoma leo Januari 20, 21. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Duwasa, Aron Joseph na Mwenyekiti wa Bodi ya Duwasa, Profesa Faustine Bee. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Kaimu Mkurugenzi wa Duwasa, Aron Joseph akizungumza kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ambaye alimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Duwasa,Prof. Faustine  Bee akiungumza na kutaja maazimio ya baraza hilo ya kuiboresha Duwasa.
Naiu Waziri wa Maji, Mhandisi Mahundi akihutubia wakati wa kuzindua  Baraza a Wafanyakazi  wa Duwasa.

Mhandisi Mahundi akijadiliana jambo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Duwasa, Aron Joseph

Sehemu ya wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Duwasa wakisikiliza kwa makini wakati Naibu waziri akihutubia.


Naibu Waziri, Mhandisi Mahundi akiwa na wajumbe wa Baraza na viongozi wa Duwasa.

 Mahundi akiagana na  wajumbe baada ya kupiga nao picha ya pamoja.


 


Na Richard Mwaikenda, Dodoma

NAIBU Waziri wa Maji, Mhandisi Maryprisca Mahundi ameitaka Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mji wa Dodoma (DUWASA), isije ikajisahau kwa kufanya kazi za menejimenti badala ya kuisimamia.

 

Naibu Waziri Mahundi ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Baraza la 6 la Wafanyakazi wa Duwasa kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), jijini Dodoma leo Januari 20, 2021.

 

Aidha, Mhandisi Mahundi amelitaka Baraza la Wafanyakazi la Duwasa kuendelea kuikumbusha Bodi kuhusu majukumu yake hayo kwa lengo la kuiendeleza mamlaka hiyo.

 

“Ni wajibu wa Taasisi za serikali  kuwa na mabaraza ya wafanyakazi kwani yameanzishwa kisheria kuishauri serikali katika ngazi ya idara, taasisi na ngazi ya wizara kuhusu usimamizi wa kazi na rasilimali watu,” amesema Naibu Waziri Mahundi.

 

Alitaja majukumu mengine ya Baraza kuwa  ni,utekelezaji wa majukumu, kulinda haki na wajibu kwa waajiri na wafanyakazi, kutoa ushauri kujenga hali bora ya kazi, maslahi bora ya wafanyakazi na kusimamia haki na usawa mahali pa kazi.

Amesema ni vyema wakachukua fursa hii  kujadiliana na kutafakari si kwa maslahi yao tu, bali utendaji wa kazi wa kila siku na jinsi ya kuboresha zaidi.

 

“Hii ni kwa sababu tija na maslahi ni matokeo ya utendaji bora unaolenga kutoa huduma bora kwa wananchi na kuchangia maslahi bora kwa watumishi,” amesema Naibu Waziri.

 

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Duwasa, Aron Joseph akizungumza kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi, amesema  lengo la mkutano huo ni kulikumbusha baraza kuhusu majukumu yao na kuwaelmisha juu sheria na utaratibu wa uendeshaji wa baraza hilo.

 

Mwenyekiti wa Bodi, Prof. Fautine Bee, alianza kwa kuwapongeza  wajumbe 63  baraza hilo la sita na kulitaka kufanya kazi kwa ushirikiano na menejimenti pamoja na wafanyakazi wa Duwasa.  kutekeleza majukumu ambayo baraza linatakiwa lifanye.

 

Prof. Bee alitaja baadhi ya maazimio waliyoafikiana kwenye mkutano huo  ili waendelee kutoa huduma iliyo bora kuwa ni; Mamlaka iendelee kutoa huduma zilizo bora, kupunguza kero kwa wananchi kuhusu upatikanaji wa maji safi na usafi wa mazingira, Kupunguza upotevu wa maji kutoka asilimia 26 kwenda chini, na kuongeza ukusanyaji mapato.

 

Mengine ni, kuhudumia wateja kwa haraka na ufanisi, kupata suluhisho la tatizo la maji chumvi, uvunaji wa maji na kuongeza kasi ya uwekezaji.


Pia wameahidi Duwasa kuwa  mamlaka bora si kwa Tanzania lakini kwa bara zima la Afrika.


IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MHARIRI BLOG YA TAIFA YA CCM
 0754264203

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages