LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 5, 2021

CCM KAKONKO, KIGOMA YAHIMIZA WAZAZI NA WALEZI KUHAKIKISHA WATOTO WALIOFAULU LASABA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA

Mbunge wa Jimbo la Buyungu Aloyce Kamamba (Wanne kutokana kulia) akiwa na Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Kakonko wakati wakikagua miradi katika jimbo hilo. 


Na Jastin Cosmas, Kakonko

Wazazi na walezi wilayani Kakonko mkoani Kigoma wamehimizwa kuhakiksha watoto walio faulu mtihani wa darasa la saba  wanaanza masomo wakiwa na mahitaji yote shule za sekondari zinapofunguliwa


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kakonko  Saamoja wakati kamati ya siasa ya wilaya ikikagua miradi mabalimbali hapa wilayani Kakonko ambapo amesisitiza suala hilo


Kwa upande wake Mbunge wa Buyungu Aloyce Kamamba amewataka Watendaji wa Kata kuwabaini Wazazi ambao wana waajiri watoto wanaopaswa kuwa shule kitendo ambacho kinarudisha nyuma elimu hivyo ametowa mwito kuhakikisha watoto walio faulu wanapelekwa shule.


Wakati huohuo Mbunge huyo ametoa kilo 100  za mchele na mabati yenye thamani ya sh. milioni 1.5 katika shule ya Sekondari Mugunzu iliyopo katika tarafa ya Kasanda ili kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa.


Aidha Katibu tarafa wa tarafa ya Kasanda Amani Kanguye akimwakilisha Mkuu wa We ya  Kakonko amesema kuwa mzazi au mlezi atakae kaidi kumpeleka mtoto shule hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages