LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 27, 2020

ZAIDI YA MADUKA 10 YATEKETEA KWA MOTO

 

Kutoka Kagera tumeamka na hii taarifa ya moto kuunguza maduka zaidi ya 10 na kuteketeza baadhi ya vitu katika majengo yanayomilikiwa na Familia ya Nekemia Kazimoto (Kazikomu) yaliyopo Mji wa kayanga mjini, Karagwe, mkabara na majengo ya city center na Magereza ya kayanga.

Moto huo umeibuka usiku wa kuamkia leo katika moja ya duka la nguo na kusambaa katika maduka mengine ya bidhaa za vyakula, hoteli, stoo za vifaa vya ujenzi, saloon na maduka ya bidhaa mchanganyiko, moto umedumu kwa zaidi masaa manne na chanzo cha moto hakijafahamika mpaka sasa.

    

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages