Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy akihutubia ka niaba ya Mkuu wa Mkoa, Dk. Binilith Mahenge wakati wa maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Nyerere Square, jijini Dodoma Desemba 1, 2020. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dodoma, Sharifa Nabalang'anya na Kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uratibu wa maandalizi ya maadhimisho hayo, Clispin Kapinga hayo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Dodoma, Sharifa
Nabalang'anya akizungumza kuhusu hatua ambazo idara hiyo inachukua kupambana
na janga hilo la Ukimwi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy ambaye
alimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Dk. Binilith Mahenge akikabidhi msaada wa pikipiki
kwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Wanaoishi na Viruzi vya Ukimwi (NACOPHA)
Konga ya Dodoma, Dorah Mwaluko kwa ajili ya kusaidia shughuli za Konga hiyo. Pikipiki
hiyo imetolewa msaada na Halmashauri ya Jiji la Dodoma wakati wa maadhimisho ya
Siku ya Ukimwi Duniani. Wa pili kulia ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii
Mkoa wa Dodoma, Sharifa Nabalang'anya
aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Jiji hilo.
Mratibu wa Huduma za Ukimwi Mkoa wa Dodoma, Dk. Abow Ahmed akisoma taarifa ya jinsi wanavyopambana kutokomeza maambukizi ya Ukimwi katika Mkoa huo ambao hivi sasa ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa maambukizi ya Ukimwi nchini.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa, Dk. Binilith Mahenge akikabidhi zawadi ya mbuzi baada ya kushinda katika mashindano ya mpira yaliyoandaliwa na kamati ya maandalizi ya maadhimisho hayo.
Wanafunzi wakisikiliza kwa makini wakati Katibu Tawala akihutubia kuhusu vijana kujiepusha na maambukizi ya Ukimwi.
Baadhi ya wafanyabiashara wakiuza bidhaa zao wakati wa maadhimisho hayo
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy, akiondoka baada ya kuhitimisha maadhimisho hayo.
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇