LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 26, 2020

TAHA KUFUNGUA FURSA ZA MASOKO, KIMATAIFA.

 



************************

Na.Mwandishi Wetu -Arusha
Asasi kilele inayojishughulisha  na masuala ya maua,matunda,mboga mboga,Mimea  itokanayo  na mizizi  na Viungo (Horticulture),imedhamiria kuendelea kukuza sekta hiyo kwa kufungua masoko ya kimataifa kwa wakulima hapa nchini.

Akizungumza na vyombo vya habari mkoani Arusha  Mkurugenzi wa TAHA dkt.Jacquline Mkindi,alisema kuwa taasisi hiyo imeandaa kongamano kubwa litakalofanyika desemba 05 jijini dar es salaam katika hoteli ya Hyatt Regency ijulikanayo Kama Kilimanjaro hoteli.

Dkt.Mkindi alisema kuwa lengo la kongamano hilo ni kuhamasisha fursa za uwekezaji wa masoko katika mazao ya horticulture na majadiliano juu ya mazingira endelevu ya kibiashara baina ya nchi zilizomo ukanda wa Afrika Mashariki na nchi za ukanda wa kusini mwa Afrika(SADC).

Aidha alisema kuwa washiriki watapata fursa ya kukutana na wadau wakubwa wa kilimo Cha horticulture kwa nchi za Afrika Mashariki pamoja na SADC ili kubadilishana uzoefu katika masuala mbalimbali ya sekta hiyo na mawazo ya kibiashara kati ya sekta binafsi na ya umma pamoja na wadau wengine kwa lengo la kuvutia wawekezaji na pia kutengeneza ushirikiano linganifu kati ya sekta ya horticulture Tanzania na zingine za kanda za kibiashara za Afrika Mashariki na Kusini.

“Naikumbukwe kuwa hivi karibuni wakati Raisi wetu Mhe.John Pombe Magufuli alitaja sekta ya horticulture kuwa miongoni mwa sekta ndogo zinazokuwa kwa Kasi nchini,ambapo alisema hivi Sasa nchi yetu inashika nafasi ya 20 kwa kuzalisha kwa wingi mazao hayo duniani na mauzo yetu ya nje yameongezeka kutoka Dola za marekani milioni 412 mwaka 2015,hadi kufikia Dola za Marekani milioni 779 mwaka 2018/2019.”Alisema dkt.
Jacquline.

Pia alisema kuwa baadhi ya maeneo ambayo yatakayojadili ni pamoja na fursa za uwekezaji,masoko,sekta ya usafirishaji,mfumo wa baridi na viwezeshi vingine vinavyosaidia upatikanaji wa masoko kama sehemu kuendeleza na kukuza kilimo na sekta hii baina ya nchi hizo.

“Naomba nitoe wito kwa Watanzania ambao ni wazalishaji, wafanyabiashara, wasafirishaji,wasindikaji,na wadau wakubwa wa horticulture kujisajili kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo wa aina yake,kupitia tovuti ya www.taha.or.tz kujifunza na kuchangamka fursa zilizopo ili kuboresha shughuli  za tasnia hii ya horticulture kisha kuendelea kuchangia ukuaji wa Uchumi nchini.”Alisema Dkt.Jacquline.

Mpaka sasa Jumla ya nchi za Tanzania ,Malawi,Rwanda,Kenya,Sudani,DRC Congo na Comoro zitashiriki  kongamano hilo,huku jumla ya washiriki 400 watahudhuria mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages