PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA, CCM BLOG.
Dk. Mary Mayige Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Nimr .Yunus Mgaya akitoa neno wakati wa maadhimisho hayo.
Wananchi wakipata huduma za upimaji wa afya wakati wa maadhimisho hayo.
Mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Francis Bujileu akielezea umuhimu wa Taasisi ya Nimr katika utafiti wa dawa za asili za kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa,Dk Selemani Serera na Monica Kessy Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa.
Mmoja wa wananchi akipima urefu ikiwa ni sehemu ya upimaji wa afya huduma ambayo ilifanyika sambamba wakati wa maadhimisho hayo.
Baadhi ya dawa ambazo NIMR inazifanyiwa majaribio na zilizofanikiwa kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu
Hotuba
ya Mh.Dr. Benilith Mahenge Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Dok. Selemani Serera wakati wa Maadhimisho ya
kumbukizi ya miaka 40 ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu
Tanzania.
Mkurugenzi
Mkuu, Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu, Tanzania
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Mkurugenzi wa NIMR kituo cha
Dodoma
Mkurugenzi Mtendaji Hospitali
ya Taifa Benjamin Mkapa.
Wageni waalikwa
Waandishi wa Habari
Mabibi na Mabwana,
Habari za asubuhi,
Nina heshima kubwa kupata fursa hii
ya kusema maneno machache katika maadhimisho haya muhimu. Awali ya yote,
napenda kuwakaribisha wote katika maadhimsho haya na napenda kutambua kazi
kubwa inayofanywa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu hasa
kwa kupambana na adui yetu mkubwa ambaye
ni magonjwa ya Binadamu.
Ni furaha yangu kubwa kuwa nanyi hapa
leo.
Mabibi na Mabwana,
Nimeelezwa kuwa Taasisi ya Taifa ya
Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu iliazishwa mwaka 1979, na ilianza kutekeleza
majukumu yake mwaka 1980. Napenda kuipongeza Taasisi hii kwa kuadhimisha umri
wa miaka 40 tangu ilivyoanza kutekeleza majukumu yake. Ikumbukwe kwamba nchi
yetu ilivopata uhuru mwaka 1961, Rais wa awamu ya kwanza Mwl.Julius Kambarage
Nyerere aliwatangazia wananchi kuwa serikali yetu inao maadui watatu wakubwa
ambao ni Umasikini, Ujinga na Maradhi, ninyi ni mashahidi
kuwa hawa maadui aliowatangaza Mwl.Nyerere mwaka 1961 bado ni maadui zetu hata
leo, magonjwa bado yapo yanasumbua binadamu na si kwa waTanzania tu bali Dunia
nzima hata nchi zilizoendelea. Nimeelezwa kuwa Taasisi hii inafanya utafiti wa
magonjwa ya Binadamu kwa nia ya kupata njia bora zaidi za kisayansi za
kukabiliana na adui magojwa kwa lengo la kuboresha afya ya watanzania na Jamii
yote kwa ujumla. Afya ya Binadamu ni muhimu sana na ni mtaji wa kwanza katika maendeleo
ya Mwanadamu, ili Dodoma na jamii yetu iweze kusonga mbele tunahitaji mazingira
salama yasiyokuwa na magonjwa pia mbinu bora na za kisayansi katika kupambana
na adui magonjwa. Kwa mantiki hiyo Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya
Binadamu mnalo jukumu kubwa kujibu
matarajio ya jamii yetu kama alivyoelekeleza Baba wa Taifa letu Mwl. Nyerere kuwa tunatakiwa kupambana
na maadui zetu hao watatu ambao nimewataja hapa awali, Taasisi hii ikifanikiwa
kupata njia bora ya kutokomeza magonjwa tayari itakuwa imeondoa umasikini
unaosababishwa na magonjwa yanayomshambulia Binadamu na kumdhoofisha kiafya,
kiuchumi na hata kusababisha kifo.
Mabibi na Mabwana, Serikali ya awamu
ya Tano inayoongozwa na Mzalendo Mwenzetu Mheshimiwa Dr.John Pombe Magufuri inalenga
zaidi katika kuimarisha miundo mbinu ya utoaji huduma za afya ya Binadamu kwa
lengo la kuwezesha kila mTanzania awe na
afya bora kwa, hivyo jukumu la Taasisi hii ni muhimu katika kutekeleza
malengo ya Serikali kwa kuwa bila utafiti hatuwezi kupata njia bora za
Kisayansi za kukabiliana na magonjwa.
Mabibi
na Mabwana, napenda nitumie fursa hii kuwapongeza Taasisi ya Taifa ya
Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu, kwa kazi kubwa mnayoifanya kutafti njia bora
za kutokomeza magonjwa, kama kifua kikuu, Ukimwi, Malaria na mengineyo, kazi
kubwa mnayoifanya ni ushahidi tosha kuwa Taasisi hii inachochea utekelezaji wa
malengo ya serikali ya awamu ya tano hongereni sana. Natumaini mnaelewa kuwa
hakuna Binadamu anaeweza kuendelea ikiwa hajaweza kudhibiti magonjwa katika
mazingira yake. Kwa hiyo ninawaagiza NIMR mfanye utafiti na kutoa suruhisho kwa
magonjwa yanayosumbua Dodoma na ikiwezekana magonjwa hayo yatokomezwe kabisa
ili katika mkoa wetu Dodoma tufanye shughuli za maendeleo tukiwa na afya njema
pasipo kukwamishwa na magonjwa.
Mabibi na Mabwana,
Leo hii tunapoadhimisha miaka 40 ya
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa
ya Binadamu Tanzania, tunatakiwa kujikita katika kufanya tafiti zenye kujibu
matatizo ya WaTanzania hususan kwa mkoa wetu wa Dodoma. Tafiti mnazozifanya
zitakuwa na tija kwa waTanzania iwapo mtalenga kupata njia bora za kutokomeza
magonjwa ambayo yanasumbua jamii yetu hivi leo, Maendeleo ya familia zetu,
jamii yetu na Taifa letu, yanategemea WaTanzania wenye afya njema. Kwa
kuzingatia majukumu ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu,
ninyi ndiyo washauri wa Serikali kuhakikisha tunapata njia bora na sahihi za
kisayansi katika kukabiliana na magonjwa, kwahiyo mnapoadhimisha miaka 40 ya
Taasisi hii muwekeze zaidi katika kuisaidia jamii yetu kupata njia bora za
kutokomeza magonjwa yote yanayoikabili jamii yetu ili tuishi katika jamii isiyo
na magonjwa.
Mabibi na Mabwana, Nitumie fursa hii kuwakaribisha Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa
ya Binadamu hapa Dodoma. Kufunguliwa kwa kituo chenu hapa Dodoma umekuja wakati
muafaka hasa ukizingatia kuwa tuna ongezeko kubwa la watu pamoja na kupanuka
kwa jiji la Dodoma, jambo ambalo mara nyingi linaambatana na mabadiliko makubwa
ikiwemo pia ongezeko la magonjwa ikiwa ni pamoja na yale yasiyoambukiza. Kwa
maana hiyo uwepo wenu hapa utakuwa na manufaa makubwa kwa wanaDodoma na Jamii
yote kwa ujumla, iwapo mtawekeza katika kutafuta mbinu bora na sahihi za kuzuia
na hata kutokomeza kabisa magonjwa haya. Kwa mantiki hiyo ninaamini
tukishirikiana vizuri nyinyi watafiti pamoja na wataalam wangu wa Afya, tutaijenga
Dodoma isiyo na Magonjwa.
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇