LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 1, 2020

RAIS MTEULE DK. MAGUFULI AKABIDHIWA CHETI CHA USHINDI WA URAIS TANZANIA

Rais Mteule Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage, katika Hafla ya kumkabidhi cheti hicho kufuatia kushinda Kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini, Jumatano, Oktoba 28, 2020. Hafla hiyo imefanyika Ofisi za Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) eneo la Njedengwa jijini Dodoma, leo, Novemba Mosi, 2020.
Dk Magufuli akionesha cheti hicho
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Makamu wa Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage.
Rais Mteule Dk. Magufuli akitoa neno la shukran.
Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi
Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama na Waliogombea Urais kupitia vyama Mbalimbali vya Upinzani nchini wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla fupi ya kukabidhi Cheti cha Ushindi.

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kiongozi wa Jopo la Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 Rais Mstaafu wa Burundi Silvestre Ntibantunganya mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage leo tarehe 01 Novemba 2020.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages