LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 15, 2020

NDEGE , HELIKOPTA KUSAIDIA KUZIMA MOTO MLIMA KILIMANJARO

 

Kilimanjaro
Image caption: Upepo na nyasi zilizokauka vimetajwa kuwa sababu ya kusambaa zaidi kwa moto katika Mlima Kilimanjaro

Serikali ya Tanzania inatazamiwa kutuma helikopta na ndege katika Mlima Kilimanjaro kusaidia kuuzima moto unaoendelea kuwaka kwa siku ya saba sasa.

Hayo ameyasema Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamis Kigwangala baada ya moto kuendelea kuwaka katika mlima huo .

Jana Waziri Kigwangala alitangaza kuwa wameweza kuudhibiti moto huo, lakini baadaye moto huo ulisaambazwa zaidi na upepo uliovuma katika mlima huo.

Katika ujumbe wake wa Twitter Waziri Kigwangala amethibitisha kuwa moto unaendela kuwaka katika mlima huo mrefu zaidi barani Afrika.

Unaweza pia kutazama:

Video content

Video caption: Washikadau wa Utalii washirikiana na serikali kuuzima moto mlima Kilimanjaro

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages