LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Oct 28, 2020

DK HUSSEIN MWINYI APIGA KURA ZANZIBAR



  1. Viongozi mbalimbali wameanza kupiga kura katika uchaguzi unaoendelea Tanzania miongoni mwao akiwa Hussein Mwinyi anayegombea urais Zanzibar.

    ''Nawapongeza Wanzanzibar wote ambao wametumia haki yao ya kupiga kura na niwaombe ambao hawajafika waendelee kujitokeza kupiga kura na hatimaye zoezi liishe kwa amani'' Bwana Mwinyi amesema.

    Video content

    Video caption: Hussein Mwinyi apiga kura yake
  2. Hali ilivyo katika baadhi ya maeneo ya kupigia kura

    Hali ilivyo katika baadhi ya maeneo ya kupigia kura
    Image caption: Hali ilivyo katika baadhi ya maeneo ya kupigia kura

    Raia nchini Tanzania wameanza kupiga kura kuchagua viongozi wao watakaowaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

    Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa kuanzia saa moja majira ya asubuhi tayari kwa zoezi hilo.

    Mwanahabari wa BBC Eagan Salla alitembelea ofisi ya mtendaji wa mtaa wa Kunduchi Mtongani eneo ambalo makarani na wasimamizi wa vituo vya kupigia kura walikuwa wanachukua vifaa, vituturi, karatasi za kupigia kura pamoja na masanduku ya kuwekea kura baada ya kura kupigwa.

    Hali imekuwa ni harakati za makarani wakiingia na kutoka eneo hilo kuelekea maeneo yao husika wanayosimamia zoezi la uchaguzi.

    Pia katika vituo vya kupigia kura muda wa mapema wakati mwanahabari Eagan Sallah anatembelea watu walikuwa sio wachache wala wengi sana wanaowasili kila mmoja kwa wakati wake wakiendelea kuhakikisha taarifa zao kwenye makaratasi ambayo yamebandikwa kwenye kuta.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages