LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 29, 2020

MSAJIRI AWAITA VIONGOZI WAKUU WA VYAMA VYOTE VYA SIASA

 

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imewaita viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa ili wazungumzie utekelezaji wa
sheria zinazosimamiwa na ofisi hiyo.

Taarifa ya ofisi hyo kwa Makatibu Wakuu wa Vyama vya Siasa vyenye usajili wa kudumu, imeeleza kuwa kikao hicho cha
viongozi wakuu wa vyama na Msajili wa Vyama vya Siasa kitafanyika Oktoba 2, mwaka huu jijini DSM.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Naibu Msajili wa Vyama Vya Siasa, Sisty Nyahoza kikao hicho kitaanza saa 2 asubuhi na
kwamba kitaanza mapema kwa kuwa Ijumaa ni siku ya ibada.

“Washiriki watakuwa ni Mwenyekiti wa Taifa na Katibu Mkuu, mnaombwa kuhudhuria bila kukosa” ilieleza taarifa hiyo iliyotolewa kwa niaba ya Msajili wa Vyama Vya Siasa.

Hivi karibuni Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilikiandikia barua Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
kuhusu kitendo cha kumnadi huko Zanzibar Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif wa
ACT-Wazalendo, kwani jambo hilo ni kinyume cha sheria.

Ofisi hiyo ilieleza kuwa kwa sasa hakuna chama chochote cha siasa, kinachoweza kushirikiana katika uchaguzi mkuu wa
mwaka huu ; na endapo kitafanya hivyo kitafanya kosa la kisheria.

Nyahoza alisema kutokana na kosa kama hilo, tayari ofisi ya msajili imekiandikia Chadema barua ya kukitaka kujieleza kwa
kitendo chake cha kumnadi Maalim Seif huko Zanzibar na pia kumnadi Zitto huko Kigoma.

“Tunataka wajieleze huo ushirikiano ukoje na ACT?” alisema kwa mujibu wa sheria, vyama hivyo kama vilitaka kushirikiana vilitakiwa kufuata utaratibu kabla ya uchaguzi, kwa maana ya kufanya mkutano wa makubaliano, waingie mkataba wa makubaliano na kuukabidhi mkataba huo wa makubaliano kwa msajili miezi mitatu kabla ya uchaguzi.

Via: HabariLE
O

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages