LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 6, 2020

TAKUKURU YAFANIKISHA KUOKOA MILIONI 29 ZILIZOKUWA ZIMETAPELIWA

  Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa mkoani Katavi imefanikiwa kurejesha kiasi cha shilingi milioni 29 za mafao ya mwalimu mstaafu Renatus Ngairo mkazi wa Kawajense katika Manispaa ya Mpanda zilizokuwa zimechukuliwa na mfanyabiashara mmoja kwa madai kuwa alikuwa akimdai mstaafu huyo
Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi; wakati wa kukabidhi kiasi hicho cha fedha; Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa katavi Christopher Nakua amesema mtuhumiwa alimnyanga’nya mwalimu huo mafao yake yote kiasi cha shilingi milioni  49 mwezi Novemba mwaka jana mara baada ya kuzitoa benki

Mkuu huyo wa TAKUKURU ameendelea kueleza kuwa mlalamikaji alifika ofisini kwao na kutoa malalamiko ambapo walianza kazi ya uchunguzi na mtuhumiwa alikiri kuwa alichukua fedha hizo kwa madai kuwa alikuwa akimkopesha mwalimu kwa muda mrefu na riba ikaongezeka

“Hata hivyo riba yenyewe haikuwa na viwango vya kueleweka hivyo mtuhumiwa amerudisha fedha taslimu shilingi milioni 24; na ameahidi kumalizia milioni tano baada ya mwezi mmoja” alisema Nakua

Kwa upande wake Mwalimu Ngairo amesema alikuwa akikopa fedha kidogo kidogo kutoka kwa mfanyabiashara huyo hadi deni lake likafikia shilingi milioni 16.4;

“Siku ya tukio alinifuata nyumbani na kuniambia mafao yako yametoka twende ukachukue fedha unilipe deni langu” alisema Ngairo

Ameendelea kueleza kuwa mara baada ya kutoa kiinua mgongo chake cha shilingi milioni 49 mtuhumiwa alimnyang’anya begi zima na kumpa milioni tatu tu

Kufuatia tukio hilo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Homera ametaka wafanyabiashara wanaokopesha kwa riba kufuata taratibu za kifedha zilizowekwa

“Hawa wamezidi sasa hapa mkoani wamekuwa wakipora fedha za watu kwa madai ya riba kuongezeka, serikali hii haitavumilia wanyonge kunyanyaswa” alisema Homera

Aidha mkuu huyo wa mkoa wa Katavi ameisifu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kutetea wanyonge

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages