LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 10, 2020

KIKUNDI CHA WAZALIWA WA KIJIJI CHA RUSOLI, MUSOMA VIJIJINI CHAENDELEA KUBORESHA UBORA WA SHULE ZA KIJIJINI MWAO

Alhamisi, 9.1.2020 Jimbo la Musoma Vijijini Kikundi cha YEBHE CHIKOMESHE kinachoundwa na baadhi ya WAZALIWA wa Kijiji cha Rusoli, Kata ya Rusoli KINAENDELEA KUCHANGIA UBORESHAJI wa Miundombinu na Vifaa vya ELIMU kwa Shule za Msingi Rusoli A&B na Rusoli Sekondari.

 Jumatatu, tarehe 6.1.2020 YEBHE CHIKOMESHE kwa kushirikiana na WADAU wao wa Maendeleo wa nchini Denmark wametoa vifaa vifuatavyo: * Computer (Desktop 1) na Photocopier 1 (+printer&scanner) kwa Rusoli Secondary School * Vifaa kama hivyo kwa S/M Rusoli A * Laptop na Projector kwa S/M Rusoli B. 

 Mbunge wa Jimbo, Prof Sospeter Muhongo aliombwa na kukubali kukabidhi vifaa hivyo kwenye Shule hizo 3 za Kijiji cha Rusoli. TUREJEE MICHANGO KUTOKA YEBHE CHIKOMESHE * Kisima cha Maji kwa ajili ya Shule zote 3 na Kijiji cha Rusoli * Vifaa vya Maabara vya Tsh Milioni 5 na Kabati la Chuma kwa Rusoli Sekondari * Nyumba ya Walimu (two in one) ya Sekondari. Ukamilishwaji unaendelea.

 * Utengenezaji wa Maktaba na Vifaa vyake kwa Shule 2 za Msingi Wananchi, Viongozi wa Chama na Serikali wanaendelea KUKISHUKURU Kikundi cha YEBHE CHIKOMESHE kwa michango ya Maendeleo wanayoitoa kwa manufaa ya JAMII nzima ya Kijiji na Kata ya Rusoli.

 TUREJEE MICHANGO KUTOKA KWA MBUNGE WA JIMBO KWA KIJIJI CHA RUSOLI (i) Madawati 64 S/M Rusoli A (ii) Madawati 97 S/M Rusoli B (iii) Mabati 50 S/M Rusoli A (iv) Mabati 54 S/M Rusoli B (v) Mbao 107 S/M Rusoli A (vi) Saruji Mifuko 60 S/M Rusoli B (vii) Saruji Mifuko 70 Rusoli Sekondari (viii) Posho ya Mwalimu wa Kujitolea wa Masomo ya Sayansi wa Rusoli Sekondari (ix) Vitabu vingi kwa Shule zote 3 (x) Vifaa vya Michezo (jezi na mipira ).

 (xi) Mbegu za Alizeti, Mtama na Mihogo Taarifa ijayo itaeleza vyanzo vya MICHANGO ya Ukamilishaji wa Chumba 1 cha Darasa kinachohitajika Rusoli Sekondari.


 Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo (katikati) akikabidhi Computers (Desktops 2 na Laptop 1), Photocopiers (2) na Projector (1) kwenye S/M Rusoli A&B na Rusoli Secondary School.
Prof. Muhongo akionesha moja ya printer iliyokabidhiwa shuleni hapo




No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages