LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 30, 2020

BAADHI YA MATAIFA YAMEANZA KUONDOA RAIA WAKE CHINA

    Virusi vya corona ambavyo vimesababisha maambukizi zaidi ya watu 7,711 na wengine 170 wamefariki nchini China,vivyo hivyo familia zinalazimishwa kutengana kutokana na mlipuko huo.
Mtaalamu wa teknolojia ya komputa ambaye ni raia wa Uingereza amejikuta anapaswa kufanya maamuzi magumu ya kumuacha mke wake ili asafiri na binti yao Jasmine mwenye umri wa miaka 9,kurejea nyumbani kwao.

Siddle na mke wake Sindy, ambaye ni raia wa China walikuwa wamesafiri na binti yao katika jimbo la Hubei ili kusheherekea mwaka mpya wa China pamoja na ndugu zake.

Hubei ni eneo ambalo watu zaidi ya 3,500 wamethibitishwa kuwa na ugonjwa huo, haswa katika mji wa Wuhan, eneo ambalo mlipuko wa ugonjwa huo ulianzia.

Mamlaka ya Japan imetoa ndege ya kwenda kuwaondoa wananchi wake katika mji wa Wuhan
Siddle anatarajiwa kusafiri Februari 1, lakini ndege zote za Wuhan zimefungiwa kutoka na serikali imefunga uwanja wa ndege na usafiri wote wa Umma pamoja na barabara kufungwa ikiwa ni jitihada ya kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.

Waliambiwa na mamlaka ya Uingereza kuwa Sindy, hawezi kuondoka licha ya kuwa na viza ya kudumu ya Uingereza tangu mwaka 2008, kwa sababu ndege hiyo ni maalum kwa ajili ya kuwaokoa raia wa Uingereza katika mji huo .

Ndege hiyo inaweza kuwasili mapema siku ya alhamisi.

"Ofisi ya mambo ya nje imetuambia kuwa ndege hiyo ni kwa ajili ya raia wa Uingereza peke yake kwa sababu mamlaka ya China inakataza raia wake kuondoka nchini humo,"Siddle aliiambia BBC.

"Ilinibidi nifanye maamuzi ya kuondoka na binti yangu ambaye ana hati ya kusafiria ya Uingereza au tubaki wote watatu."

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages