LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 24, 2019

JESHI LA POLISI LAMNASA MKUFUNZI ALIYESABABISHA MAUAJI

  Polisi Mkoani Singida wanamsaka Mkufunzi Msaidizi wa Jeshi la Akiba Said Ng'imba kwa tuhuma za mauaji ya Vijana wawili waliokuwa kwenye mafunzo ya Jeshi la Mgambo Kata ya Mudida Singida.

Kamanda wa Polisi Singida, Sweetbert Njewike amesema Wanafunzi hao wanadaiwa kufariki baada ya kupewa adhabu iliyopitiliza kwa kutakiwa watumbukie ndani ya dimbwi lililojaa maji ya mvua kitendo kilichopelekea wapoteze maisha kwa kushindwa kupumua.

Inadaiwa Mkufunzi aliwapa adhabu hiyo baada ya Wawili hao kutuhumiwa kutoshiriki ipasavyo mafunzo ya November 19 mwaka huu.

"Wanafunzi hao baada ya kutumbukia kwenye maji hawakuibuka, Mkufunzi akatoweka haraka na kukimbiia kusikojullikana, tunaendelea kumsaka"-Amesema

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages