LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 30, 2019

ALI KIBA ASHIRIKI MBIO ZA TABORA GREEN MARATHON


 Na,Editha Edward –Tabora 

Msanii wa bongo fleva Ally Salehe Kiba Maarufu kama Alikiba ameshiriki mbio za Tabora green marathon kwa kukimbia km 2.5 zilizoanzia ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora hadi viwanja vya Ali Hassan Mwinyi zilizofanyika hii leo mkoani humo 

Akizungumza katika mbio hizo msanii alikiba amesema mbio zimemfanya achangamshe mwili na akili kwani michezo zinajenga urafiki pia zinakutanisha watu na zinaimarisha mwili hivyo amefurahi kushiriki pamoja na mkuu wa mkoa huo na amewahimiza wananchi wa mkoa huo kuwa na utamaduni wa kukimbia ma kufanya mazoezi ili waweze kuwa imara kimwili.

 Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri naye alikuwa ni miongoni mwa wakimbia mbio hizo ambapo yeye amekimbia mbio umbali wa km2.5 ambapo amesema msanii alikiba ni mfano wa kuigwa kwani tangu afike mkoani humo katika tamasha lake la muziki linalojulikana kama unfogetabletour ameweza kufanya mambo mengi ya kijamii ‘’Msanii.

Pichani ni Msanii Wa bongo fleva Alikiba na mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakikimbia mbio za Tabora Green Marathon 
Pichani ni Msanii Wa bongo fleva Alikiba na mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakikimbia mbio za Tabora Green Marathon 
Pichani ni Msanii Alikiba akimvalisha medani mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri baada ya kukimbia mbio za km 2.5
Msanii Alikiba akipanda mti nje ya uwanja wa Ali Hassan Mwinyi baada ya kukimbia mbio.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages