Rais Yoweri Museven wa Uganda ameitaka Russia kupanua zaidi ushirikiano wake na mataifa ya Afrika huku akiipongeza nchi hiyo kutokana na juhudi zake za kusaidia harakati za kujikomboa za nchi za bara hilo.
Rais Museven ameyasema hayo kando na mkutano uliowakutanisha viongozi wa nchi za Afrika na Rais Vladmir Putin wa Russia katika mji wa bandari wa Sochi. Aidha Museven kama walivyofanya marais wengi wa Afrika alimtaka Rais Putin kuiuzia silaha na zana za kisasa za kijeshi nchi yake.

Katika hatua nyingine jeshi la Uganda limefanya kikao maalumu na wakuu wa idara za usalama kujadili njia za kukabiliana na ongezeko la matukio ya wizi na ujambazi ndani ya nchi hiyo mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwa maelezo zaidi jiunge na mwandishi wetu wa mjini Kampala, Kigozi Ismail kwa kubonyeza alama ya sauti pale juu……………/
No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇