Rais FĂ©lix Antoine Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameanzisha mazungumzo na marais wa Rwanda na Uganda kwa lengo la kuwarejesha nchini waazi wa M23 waliokimbilia nchi hizo hapo mwaka 2013.
Rais Tshisekedi amechukua hatua hiyo ikiwa ni katika ajenda yake ya kurejesha usalama na amani katika maeneo ya mikoa ya mashariki mwa nchi hiyo ambayo kwa muda sasa imekuwa ikishuhudia mauaji na machafuko.
Kwa mujibu wa mpango huo, kurejeshwa usalama huko mashariki mwa Kongo DR, kunahitajia kualikwa askari wa Rwanda na Uganda kushiriki katika operesheni za kuwasaka waasi wa maeneo hayo, suala ambalo linatajwa kuwa huwenda likawa njia mjarabu ya kuhitimisha hali ya mchafukoge katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇