Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani amewasha rasmi umeme katika kijiji cha Nyakabwera wilayani Kyerwa na Nyarugondo wilayani Karagwe, Mkoa wa Kagera, tukio lililoibua furaha kwa wakazi wa vijiji hivyo.
Akiwa amefuatana na viongozi na wataalamu mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa; Waziri aliwasha umeme katika maeneo hayo na kuzungumza na wananchi, akiwa katika ziara ya kazi, jana, Julai 18, 2019.
“Nampongeza Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli; anafanya kazi kubwa. Katika sekta ya nishati, amedhamiria kufikisha umeme katika vijiji vyote nchini,” Waziri Kalemani aliwaambia wananchi.
Kabla hajawasha rasmi umeme katika vijiji hivyo, Waziri alitoa hamasa kwa wananchi wa maeneo husika ambao hawajaunganishiwa umeme, kuchangamkia fursa hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kulipia gharama inayohitajika ambayo ni shilingi 27,000 ili wote wawe na umeme.
Vilevile, aliwataka kulinda miundombinu ya umeme iliyopo katika maeneo yao ili kuiwezesha serikali kuendelea kuwapatia huduma hiyo kwa ufanisi.
Alisema atakayebainika kuhujumu miundombinu hiyo, atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Pia, aliwashauri viongozi wa taasisi za umma pamoja na miradi mbalimbali ya kijamii kama vile mitambo ya maji, shule, vituo vya afya, masoko, nyumba za ibada na kadhalika, kutenga fedha za kulipia huduma ya kuunganishiwa umeme ili nishati hiyo ipelekwe katika maeneo hayo muhimu.
Akiwa amefuatana na viongozi na wataalamu mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa; Waziri aliwasha umeme katika maeneo hayo na kuzungumza na wananchi, akiwa katika ziara ya kazi, jana, Julai 18, 2019.
“Nampongeza Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli; anafanya kazi kubwa. Katika sekta ya nishati, amedhamiria kufikisha umeme katika vijiji vyote nchini,” Waziri Kalemani aliwaambia wananchi.
Kabla hajawasha rasmi umeme katika vijiji hivyo, Waziri alitoa hamasa kwa wananchi wa maeneo husika ambao hawajaunganishiwa umeme, kuchangamkia fursa hiyo kwa kujitokeza kwa wingi kulipia gharama inayohitajika ambayo ni shilingi 27,000 ili wote wawe na umeme.
Vilevile, aliwataka kulinda miundombinu ya umeme iliyopo katika maeneo yao ili kuiwezesha serikali kuendelea kuwapatia huduma hiyo kwa ufanisi.
Alisema atakayebainika kuhujumu miundombinu hiyo, atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Pia, aliwashauri viongozi wa taasisi za umma pamoja na miradi mbalimbali ya kijamii kama vile mitambo ya maji, shule, vituo vya afya, masoko, nyumba za ibada na kadhalika, kutenga fedha za kulipia huduma ya kuunganishiwa umeme ili nishati hiyo ipelekwe katika maeneo hayo muhimu.

No comments:
Post a Comment
Tupia Comments👇