LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 25, 2019

WATU WASIOPUNGUA 6 WAUAWA NA MEYA WA MOGADISHU AJERUHIWA KATIKA MLOPUKO WA BOM

Mohamed Abdi Hayir Waziri wa Habari wa Somalia amesema kuwa Meya Abdirahman Omar Osman amejeruhiwa vibaya katika mlipuko huo. Makamishna wawili wa wilaya na wakurugenzi watatu wa mikoa pia ni miongoni mwa watu waliouliwa katika mlipuko huo wa Mogadishu. Kundi la kigaidi la al Shabaab lenye makao yake huko Somalia limedai kuhusika na shambulio hilo la bomu la kujilipua na kusema kuwa shambulio hilo lilikusudiwa kuwalenga maafisa wa Umoja wa Mataifa ambao walikuwa wakilizuru jengo hilo la serikali.
Meya wa Mogadishu, Abdirahman Omar Osman ambaye amejeruhiwa vibaya katika mlipuko wa bomu 

Masaa machache kabla ya mlipuko huo wa bomu, James Swan Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Somalia ambaye pia ni mwanadiplomasia wa Marekani alikuwa amekutana na kufanya mazungumzo na Meya wa mji mkuu Mogadishu pamoja na makamishna wake wa wilaya katika jengo hilo la serikali; lakini aliondoka baada ya mazungumzo hayo. Swan amesema analaani shambulio hilo la kutisha ambalo si tu linadhihirisha kutoheshimu na kujali maisha ya watu lakini pia ni shambulio ambalo linawalenga wananchi wa Somalia wanaofanya juhudi za kuboresha maisha ya Wasomali wenzao katika eneo la Banadir katika mji mkuu Mogadishu.

No comments:

Post a Comment

Tupia Comments👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages