LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 24, 2019

SERIKALI YAKERWA NA VITENDO VYA USHIRIKINA

SALVATORY NTANDU

Serikali wilayani Kahama imesema itaweka ulinzi katika njia panda inayoelekea katika nyumba ya mkuu wa walaya ya kahama mkoani shinyanga ambayo inatumika kufanyia vitendo vya ushirikina baada ya kukithiri kwa vitendo vya kishirikina katika eneo hilo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake baada ya kuongezeka kwa matukio hayo na kusema kuwa wataweka walinzi maalum katika eneo hilo ili kuwabaini watu wanaotekeleza vitendo hivyo.

Amesema mbali na kufanya vitendo hivyo ambavyo havifai kwenye jamii wahusika wamekuwa wakiharibu barabara na mazingira kwa kutupa vitu mbalimbali katika eneo hilo pindi wanapomaliza kufanya kafara zao kama vile nazi,kuku,mbuzi hali ambayo haitaweza kuvumilika.

Amefafanua kuwa jamii inapaswa kuachana na vitendo hivyo vya upigaji wa ramli chonganishi hivyo ni budi wakafanya kazi halali za kuwapatia vipato halali na kuachana na imani potofu za kishirikina zinazofanywa na waganga wakienyeji katika eneo hilo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages