LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jun 29, 2019

NAOMBA RADHI KWA RAIS NA WATANZANIA WOTE

Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars, Paul Makonda amemuomba radhi Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, John Pombe Magufuli kufuatia Stars kupoteza mechi ya pili mfululizo.

Makonda ameomba radhi hiyo jijini Cairo kwamba kila Mtanzania alikuwa na imani ya kupata ushindi katika mchezo wa jana dhidi ya Harambee Stars ambapo Stars ilifungwa bao 3-2.

Makonda amesema Watanzania wanapaswa kuendelea kuiombea timu yao na kuiunga mkono kwani matokeo hayo ni sehemu ya mchezo.

Mkuu huyo alisema licha ya Stars kupoteza ameridhika na jinsi kikosi hicho kilivyocheza kwa nguvu ikiwa ni tofauti na mchezo wa kwanza waliofunga na Senegal bao 2-0.

No comments:

Post a Comment

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages