Watu wanne zaidi wameripotiwa kupoteza maisha katika mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Ugonjwa wa Ebola ulianza tena Julai 2018 na kusababisha vifo vya watu 655 huku wengine 345 waliokuwa na virusi wakiwa wamepona kabisa.
Kwa upande mwingine, kwa mujibu wa data, watu 66 wamethibitishwa kupoteza maisha kutokana na homa iliyosababishwa an virusi hivyo.
Chini ya kampeni iliyozinduliwa tarehe 8 Agosti mwaka wa 2018 watu 96,136 wamepatiwa chanjo.
Ebola, kwa mara ya kwanza ililipuka mwaka 1976.
Virusi vya Ebola viliennea Afrika Magharibi mnamo Desemba 2013.
Mwaka 2014-2017 nchini Ginea, Liberia na Sierra Leone, watu elfu 30 waliambukizwa na zaidi ya watu 11,000 walikufa.
No comments:
Post a Comment
MAONI (COMMENTS)👇