LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Mar 30, 2019

SHERIA MPYA YAJA KULINDA RASILIMALI ZA TANZANIA


WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba John Kabudi amesema mabadiliko ya sheria yaliyofanyika hivi karibuni katika sekta za madini, maliasili na uwekezaji yana lengo la kuweka mazingira bora yatakayoleta tija kwa Taifa na wawekezaji kuondoa utaifishaji (nationalization) na upokonyaji mali (confiscation).

Kabudi (kulia), meyasema hayo wakati wa mazungumzo na Mwenyekiti wa Taasisi ya Africa Matters Limited Lynda Chalker (kushoto) na kuongeza kuwa hatua zilizochukuliwa na serikali ya awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dkt John Pombe Magufuli ni kuweka uwanda sawa kwa kuondoa rushwa na urasimu na kumtaka Mhe Chalker kuhamasisha wawekezaji kutoka Uingereza kuja kuwekeza hapa nchini.

Katika mazungumzo hayo Profesa Kabudi amemuahakikishia Mwenyekiti huyo wa Taasisi ya  Africa Matters limited kuwa mazingira ya uwekezaji nchini ni salama na yameboreshwa zaidi na hakuna masuala ya utaifishaji (nationalisation) wala upokonyaji mali (confiscation) kama inavyopotoshwa na baadhi ya watu wasioitakia mema Tanzania.

“Katika kutekeleza diplomasia ya Uchumi Tanzania inatoa kipaumbele kwa uwekezaji wenye tija kwa Taifa na unaozingatia maslahi ya pande zote (Win – win situation) kwa kuwa sasa kupitia sheria mpya tuna mfumo wa kodi unaofahamika, misamaha ya kodi isiyo na upendeleo na si kweli kuwa mazingira yamebadilika na kusema kweli kilichbadilika ni usimamizi madhubuti,kupambana na rushwa na kuhakikisha kodi stahiki inalipwa” Amesema Kabudi

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Africa Matters Limited Lynda Chalker amempongeza Rais Dkt Magufuli kwa kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini na kuongeza kuwa atakaporejea Uingereza msafara wa wafanyabiashara na wawekezaji kuja Tanzania na kwamba kuna uwezekano mkubwa wa uwepo wa mabadiliko ya kisiasa nchini Uingereza na marafiki wa Jumuia ya madola kama Tanzania wanapewa kipaumbele katika uwekezaji na ujenzi wa viwanda.

“Ninadhani wawekezaji hasa wa nje ya Tanzania wanahitaji kufanya utafiti kidogo kuhusu kile Tanzania inachokihitaji na namna  watakavyonufaika kwa kuwekeza Tanzania,nimuahidi waziri hapa kuwa nitakaporejea London, nitakutana na mjumbe maalum wa Uingereza wa mambo ya biashara kwa Tanzania pia nitaonana na mawaziri wa mambo ya nje wa Uingereza na Jumuia ya Madola kuona  uwezekano wa kuwa na mkutano mkubwa ambao utazungumzia zaidi masuala ya uwekezaji na biashara kwa Tanzania”


1 comment:

  1. TIC ifike huku vijijini tupo wakulima wadogo wenye ekari kati ya hamsini na mia ambao tungependa kushirikiana na wawekezaji wa kati katika ufugaji na ukulima wa organic wa mboga,kuku,etc

    ReplyDelete

MAONI (COMMENTS)👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages