• Home
  • About CCM's Official Blog
  • Contact/Mawasiliano

CCM Blog
    • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • KIJAMII
    • SIASA
    • BIASHARA
    • UCHUMI
    • MICHEZO
    • BURUDANI
    • MAKALA
    • MAGAZETI
  • LATEST HEADLINES👉

    Your Ad Spot

    Mar 18, 2019

    Home siasa MAALIM SEIF AZIKANA MALI ZA CUF ZANZIBAR BAADA YA KUTIMKIA ACT-WAZALENDO

    MAALIM SEIF AZIKANA MALI ZA CUF ZANZIBAR BAADA YA KUTIMKIA ACT-WAZALENDO

    CCM Blog March 18, 2019 ,siasa



    Maalim Seif Sharif Hamad

    Dar es Salaam, TANZANIA.
    Mali za Chama Cha Civic United Front  (CUF) Zanzibar zimeingia kwenye utata baada ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad kuhamia chama cha ACT-Wazalendo.
    Utata na hatma ya mali hizo unafuatia Katibu Mkuu huyo kuzikana mali za CUF zikiwemo ofisi za makao makuu ya chama hicho zilizopo Zanzibar akidai kuwa ofisi hizo zilikodiwa na hazikuwa mali ya chama.
    Maalim amesema hatma ya umiliki wa majengo hayo ipo mikononi mwa mmiliki wa majengo hayo.
    Maalim ametangaza kujiunga na ACT-Wazalendo leo Jumatatu, Machi 17, 2019 kwenye mkutano na Waandishi wa habari uliofanyika kwenye ofisi za wabunge wa CUF zilizopo Magomeni, jijini Dar es Salaam.
    Uamuzi huo wa gwiji hilo la siasa nchini Tanzania umekuja saa chache tu baada ya Mahakama Kuu nchini Tanzania kumthibitisha Haruna Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa chama hicho.
    Uamuzi huo wa mahakama kuu wa kumtambua Lipumba ulileta taharuki kwa wafuasi wa CUF wanaomuunga mkono Maalim ambao walikuwa hawamtaki Lipumba.
    Maalim amesema yeye na viongozi wenzake wamefikia maamuzi hayo ya kujiunga na ACT baada ya kuvitembelea vyama kadhaa vya siasa kabla hawajafanya maamuzi ya kujiunga na ACT – Wazalendo.
    Kiongozi huyo aliyekuwa mgombea wa CUF nafasi ya Urais Zanzibar tangu mwaka 1995, amewataka wanachama wote wa CUF wanaomuunga mkono kujiunga na ACT – Wazalendo.
    “Nyumba uliyoizoea ni ngumu kuihama. Ila inafika mahala lazima ufanye maamuzi. Tumeamua kuiacha nyumba yetu ya zamani na sasa tupo kwenye nyumba mpya.
    “Tulichofanya ni kushusha nanga na kuong’oa nanga. Dhamira yetu ya mapambano ipo pale pale ila sasa tunayafanya kwenye chombo kingine,” amesema Maalim Seif.
    Kwa habari zaidi soma link ifuatayo;
    Tags siasa#
    Share This
    Author Image

    About CCM Blog

    siasa
    By Blog CCM Blog CCM Blog - March 18, 2019
    Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
    Tags siasa

    No comments:

    Post a Comment

    Tupia Comments👇

    Newer Post Older Post Home
    Subscribe to: Post Comments (Atom)

    Post Top Ad

    Your Ad Spot

    KWAKO MTANZANIA

    KWAKO MTANZANIA

    ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA 2025/30

    ILANI YA UCHAGUZI YA CHAMA CHA MAPINDUZI YA 2025/30

    VIONGOZI WAKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

    VIONGOZI WAKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
    Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Rais Dk. Samia Suluhu Hassan

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM ZANZIBAR

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM ZANZIBAR
    Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, BARA

    MAKAMU MWENYEKITI WA CCM, BARA
    Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Steven Wasira

    KATIBU MKUU WA CCM

    KATIBU MKUU WA CCM
    Balozi Dk. Asha-Rose Migiro

    Chagua Lugha/Translate Language👇





    Tafuta (Search) hapa👇

    CCM Blog. Powered by Blogger.

    Pages

    • Home


    Idadi ya wanaosoma CCM Blog

    Tuma Ujumbe hapa

    Name

    Email *

    Message *

    This Blog Designed and Developed By Bashir Nkoromo | Bashir Nkoromo | Property of Chama Cha Mapinduzi