LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 27, 2018

TANZANIA YAPONGEZWA NA CDC UFUATILIAJI, UTOAJI TAARIFA ZA MAGONJWA KIMATAIFA

 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akiongea na wadau wa Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto katikati   akimsikiliza kwa makini na Mkurugenzi Mkuu wa  Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) Dkt. Robert Redfild kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini , katikati ni Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania Balozi Inmi Petterson.
 Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu kushoto akifatilia takwimu zinazotolewa na mfumo wa ufatiliaji wa magonjwa nchini pamoja  na wadau wa Kituo cha Kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) wakati wa kikao  kuhusu hali ya utekelezaji katika kufuatilia, kutoa taarifa na kudhibiti magonjwa nchini.

Mtaalamu wa kitengo cha mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa nchini Dkt. Ally Nyangi akitoa maelezo kwa Wadau wa Kituo cha kimataifa cha kudhibiti magonjwa (CDC) hawapo pichani kuhusu jinsi mfumo huo unayofanya kazi nchini.



TANZANIA imepata pongezi kutoka kwa Kituo cha Kimataifa cha kufuatilia , kutathimini , kutoa taarifa na kuchukua hatua (CDC) kwa kufanya vizuri katika utekelezaji huo hasa katika magonjwa ya mlipuko. 
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu  wakati wa kikao cha kuangalia hali ya utendaji katika sekta ya Afya nchini. 
"Wenzetu wa CDC kutoka  Marekani wanatusaidia kujenga uwezo wa kufuatilia , kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa ya mlipuko kama vile Ebora na Kipindupindu na wameridhika kwa utendaji wetu hapa nchini" alisema Waziri Ummy. 
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Tanzania imeimarika katika kufanya uchunguzi , kutathimini ,  kutoa taarifa na kuchukua hatua juu ya magonjwa mbalimbali. 
Mbali na hayo Waziri Ummy amesema  kuwa magonjwa hayana mipaka hivyo ni lazima kuwa waangalifu na  kuchukua hatua mda wote kwa kujenga mifumo imara ya ufuatiliaji. 
Kwa upande wake  Kaimu Balozi wa Marekani Nchini Bi. Inmi Petterson amesema kuwa wamefurahishwa na kazi ya wataalamu wa afya waliowekwa hapa nchini katika kupambana na magonjwa na kuahidi kuongeza nguvu kubwa ikiwemo vitendea kazi. 
Aidha Balozi Inmi amesesema kuwa Serikali ya Tanzania inatakiwa kushirikiana na wananchi wa Tanzania katika kupata taarifa sahihi za magonjwa na kujenga nchi yenye wananchi wenye afya bora. 

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages