HABARI MPYA

Your Ad Spot

Apr 22, 2018

MASHINDANO YA OLIMPIKI 2020 NCHINI JAPAN KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII VYA TANZANIA - DK. KIGWANGALLA





Na Hamza Temba-Ngorongoro, Arusha
Mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika nchini Japan mwaka 2020 yatatumika kunadi vivutio vya utalii vya Tanzania kupitia timu ya Taifa ya riadha na banda la maonesho ya utalii.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na wananchi muda mfupi baada ya kukamilika kwa mashindano ya riadha ya Ngorongoro Marathon 2018 katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana.

Dkt. Kigwangalla alitoa kauli hiyo wakati akijibu ombi la Rais wa Chama cha Riadha Tanzania, Anthony Mtaka ambaye aliiomba wizara yake kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kusaidia maandalizi ya timu ya Taifa ya riadha itakayoshiriki mashindano hayo.

Mtaka pia aliomba Mamlaka hiyo itumie timu ya Taifa ya riadha Tanzania kama mabalozi wao wa kutangaza vivutio vya utalii vya hifadhi hiyo ya Ngorongoro ndani na nje ya nchi.

Akijibu maombi hayo, Dk. Kigwangalla alisema kitaundwa kikosi kazi cha pamoja kati ya wizara yake kupitia taasisi zake hususan Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro na Chama cha Riadha Tanzania ili kuainisha mahitaji ya mashindano hayo na kuweka makubaliano yatakayonufaisha pande zote.

"Kama tunaweza kupata jukwaa la nchi zaidi ya 50 au 100 kwa kufadhili wanariadha 200 kwenda kushiriki, manake hilo jukwaa linatulipa, kwa sababu tunawekeza kidogo tunaonekana kwa kiasi kikubwa.

"Mwaka 2020 kwenye Olimpiki lazima tuwekeze, na sisi Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia taasisi zetu tutapenda tuunde kikosi kazi cha pamoja ili tuangalie gharama zinazohusika, maandalizi yanayohitajika ili na sisi kama Wizara kupitia taasisi zetu kama Ngorongoro tuweze kuona nini mchango wetu, lakini sisi tutataka tujue faida yetu hasa itakuwa ni nini" alisema Dk. Kigwangalla.

Alisema mashindano hayo yatatoa fursa pana kwa Taifa kutangaza vivutio vyake mbali na juhudi zinazofanywa hivi sasa kupitia maonesho ya kimataifa. "Kupitia mashindano hayo tutapeleka pia maombi kwenye ofisi ya balozi wetu nchini Japan ili tupewe banda la kunadi vivutio vyetu vya utalii" alisema.

Dk. Kigwangalla pia aliitaka Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kukubali ombi la Chama cha Riadha Tanzania la kuanzisha kituo cha mafunzo ya riadha mjini Karatu ili kuimarisha mchezo huo na timu ya riadha Tanzania sambamba na kutumia kituo hicho kama fursa ya kutangaza utalii wa hifadhi hiyo.

Alisema kituo hicho pia kijengwe sanamu za wanariadha mashuhuri waliowahi kuiletea sifa Tanzania na kuweka rekodi mbalimbali ili kutoa motisha kwa wanariadha wengine wanaochipukia.

Alisema mbali na kuanzisha kituo hicho, timu hiyo ya Riadha Tanzania inaweza pia kupewa jina la Ngorongoro ili kuitangaza hifadhi hiyo yenye vivutio vya kipekee duniani ambavyo vimeifanya itambulike kama sehemu ya urithi wa dunia.

Mashindano ya Ngorongoro Marathon kwa mwaka huu 2018 yamehusisha washikiri kutoka Tanzania na Kenya ambapo washindi wa kwanza wa mbio hizo za kilomita 21 upande wanaume na wanawake wametoka nchini Kenya. Kaulimbiu ya mashindano hayo imelenga kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimsalimia Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dkt. Fredy Manongi muda mfupi kabla ya kuanza kwa mashindano hayo. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Waziri Kigwangalla akiwa tayari kuzindua mashindano hayo katika umbali wa kilomita 21.
Washiriki wa mbio hizo kutoka Tanzania na Kenya wakitimua mbio kuanza mashindano hayo ya Ngorongoro Marathon 2018 umbali wa Kilomita 21 mjini Karatu mkoani Arusha. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Baadhi ya watalii nao walitumia fursa hiyo kusaka medali.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Baadhi ya washiriki wa mashindano hayo wakiwa katika harakati za kusaka medali.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akihitimisha mbio za kilomita 21 za mashindano ya Ngorongoro Marathon 2018 yaliyofanyika katika mji wa Karatu mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Haikuwa kazi rahisi, washiriki wengine walilazimika kuvua viatu na kuvaa kandambili ili kurahisiha kazi yao ya kutafuta medali.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akionesha medali aliyopewa pamoja na washiriki wengine wa mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 yaliyofanyika mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. 
 Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki nchini Tanzania, Filbert Bayi akizungumza wakati wa hafla hiyo.
 Rais wa Chama cha Riadha Tanzania, Anthony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akitoa salamu zake katika hagla hiyo ambapo ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kufadhili mashindano hayo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mfaume Taka akizungumza na wananchi muda mfupi baada ya kumalizika kwa mbio hizo mjini Karatu.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kuhitimisha mashindano hayo mjini Karatu.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi cheti cha shukurani Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dkt. Fredy Manongi kwa kufanikisha mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi milioni moja mshindi wa kwanza wa kilomita 21  kwa wanawake, Monica Chemko kutoka Kenya katika mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi milioni moja mshindi wa kwanza wa kilomita 21  kwa wananume, Joseph Patha kutoka Kenya katika mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wengine wa mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 yaliyifanyika mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. 
KAWAIDA MASHINDANO YA OLIMPIKI 2020 NCHINI JAPAN KUTANGAZA VIVUTIO VYA UTALII VYA TANZANIA - DK. KIGWANGALLA Na Hamza Temba-Ngorongoro, Arusha ..................................................................................... Mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika nchini Japan mwaka 2020 yatatumika kunadi vivutio vya utalii vya Tanzania kupitia timu ya Taifa ya riadha na banda la maonesho ya utalii. Hayo yameelezwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na wananchi muda mfupi baada ya kukamilika kwa mashindano ya riadha ya Ngorongoro Marathon 2018 katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana. Dkt. Kigwangalla alitoa kauli hiyo wakati akijibu ombi la Rais wa Chama cha Riadha Tanzania, Anthony Mtaka ambaye aliiomba wizara yake kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kusaidia maandalizi ya timu ya Taifa ya riadha itakayoshiriki mashindano hayo. Mtaka pia aliomba Mamlaka hiyo itumie timu ya Taifa ya riadha Tanzania kama mabalozi wao wa kutangaza vivutio vya utalii vya hifadhi hiyo ya Ngorongoro ndani na nje ya nchi. Akijibu maombi hayo, Dk. Kigwangalla alisema kitaundwa kikosi kazi cha pamoja kati ya wizara yake kupitia taasisi zake hususan Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro na Chama cha Riadha Tanzania ili kuainisha mahitaji ya mashindano hayo na kuweka makubaliano yatakayonufaisha pande zote. "Kama tunaweza kupata jukwaa la nchi zaidi ya 50 au 100 kwa kufadhili wanariadha 200 kwenda kushiriki, manake hilo jukwaa linatulipa, kwa sababu tunawekeza kidogo tunaonekana kwa kiasi kikubwa. "Mwaka 2020 kwenye Olimpiki lazima tuwekeze, na sisi Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia taasisi zetu tutapenda tuunde kikosi kazi cha pamoja ili tuangalie gharama zinazohusika, maandalizi yanayohitajika ili na sisi kama Wizara kupitia taasisi zetu kama Ngorongoro tuweze kuona nini mchango wetu, lakini sisi tutataka tujue faida yetu hasa itakuwa ni nini" alisema Dk. Kigwangalla. Alisema mashindano hayo yatatoa fursa pana kwa Taifa kutangaza vivutio vyake mbali na juhudi zinazofanywa hivi sasa kupitia maonesho ya kimataifa. "Kupitia mashindano hayo tutapeleka pia maombi kwenye ofisi ya balozi wetu nchini Japan ili tupewe banda la kunadi vivutio vyetu vya utalii" alisema. Dk. Kigwangalla pia aliitaka Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro kukubali ombi la Chama cha Riadha Tanzania la kuanzisha kituo cha mafunzo ya riadha mjini Karatu ili kuimarisha mchezo huo na timu ya riadha Tanzania sambamba na kutumia kituo hicho kama fursa ya kutangaza utalii wa hifadhi hiyo. Alisema kituo hicho pia kijengwe sanamu za wanariadha mashuhuri waliowahi kuiletea sifa Tanzania na kuweka rekodi mbalimbali ili kutoa motisha kwa wanariadha wengine wanaochipukia. Alisema mbali na kuanzisha kituo hicho, timu hiyo ya Riadha Tanzania inaweza pia kupewa jina la Ngorongoro ili kuitangaza hifadhi hiyo yenye vivutio vya kipekee duniani ambavyo vimeifanya itambulike kama sehemu ya urithi wa dunia. Mashindano ya Ngorongoro Marathon kwa mwaka huu 2018 yamehusisha washikiri kutoka Tanzania na Kenya ambapo washindi wa kwanza wa mbio hizo za kilomita 21 upande wanaume na wanawake wametoka nchini Kenya. Kaulimbiu ya mashindano hayo imelenga kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimsalimia Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dkt. Fredy Manongi muda mfupi kabla ya kuanza kwa mashindano hayo. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri Kigwangalla akiwa tayari kuzindua mashindano hayo katika umbali wa kilomita 21. Washiriki wa mbio hizo kutoka Tanzania na Kenya wakitimua mbio kuanza mashindano hayo ya Ngorongoro Marathon 2018 umbali wa Kilomita 21 mjini Karatu mkoani Arusha. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Baadhi ya watalii nao walitumia fursa hiyo kusaka medali. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Baadhi ya washiriki wa mashindano hayo wakiwa katika harakati za kusaka medali. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishiriki mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 na wanariadha wengine mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akihitimisha mbio za kilomita 21 za mashindano ya Ngorongoro Marathon 2018 yaliyofanyika katika mji wa Karatu mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Haikuwa kazi rahisi, washiriki wengine walilazimika kuvua viatu na kuvaa kandambili ili kurahisiha kazi yao ya kutafuta medali. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akionesha medali aliyopewa pamoja na washiriki wengine wa mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 yaliyofanyika mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Katibu Mkuu wa Kamati ya Olimpiki nchini Tanzania, Filbert Bayi akizungumza wakati wa hafla hiyo. Rais wa Chama cha Riadha Tanzania, Anthony Mtaka ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu akitoa salamu zake katika hagla hiyo ambapo ameipongeza Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kufadhili mashindano hayo. Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mfaume Taka akizungumza na wananchi muda mfupi baada ya kumalizika kwa mbio hizo mjini Karatu. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akizungumza katika mkutano wa hadhara wa kuhitimisha mashindano hayo mjini Karatu. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi cheti cha shukurani Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro, Dkt. Fredy Manongi kwa kufanikisha mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi milioni moja mshindi wa kwanza wa kilomita 21 kwa wanawake, Monica Chemko kutoka Kenya katika mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimkabidhi milioni moja mshindi wa kwanza wa kilomita 21 kwa wananume, Joseph Patha kutoka Kenya katika mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 zilizofanyika katika mji wa Karatu, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha jana. Kaulimbiu ya mashindano hayo na kupiga vita ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wengine wa mashindano ya mbio za Ngorongoro Marathon 2018 yaliyifanyika mjini Karatu mkoani Arusha jana ambapo alimaliza mbio hizo kwa kukimbia kilomita 21.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages