Na Charles Charles
Inawezekana kweli alikwenda. Lakini hii lugha ya kwamba eti "amevamia" ama "ameteka" ni kuongeza chumvi.
Hivi panapovamiwa au kutekwa kunakuwa hakuna purukushani, hakuna majeruhi hata mmoja wala patashika ya aina yoyote?
Pili,
kwa nini inasemwa kwamba alikwenda na askari/wanajeshi wenye silaha
wakati picha ile anaonekana afisa usalama mmoja tu ndiye ana bunduki?
Mbona yule askari polisi hana hata manati, lakini tunaambiwa "watu wenye silaha" utadhani zaidi ya mmoja?
Tatu,
mbona mara nyingi tunaona wakuu wa mikoa wanapokwenda "site" huwa
wamezungukwa ama kulindwa na polisi, tena zaidi ya mmoja huku wamebeba
bunduki na mchana kweupe? Nani kati yetu aliyewahi kulihoji hili?
No comments:
Post a Comment
ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇