LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Aug 6, 2014

SUMATRA YAHAMASISHA MATUMIZI YA MITUMBWI YA KISASA ILI KUPUNGUZA AJALI MAJINI



Adam Mamilo Afisa udhibiti vyombo vya majini Wilaya ya Kyela  akitoa maelezo kwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Mbeya walipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika Maonyesho ya Sherehe za wakulima Nane nane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini kuhusiana na  matumizi ya  mitumbwi ya kisasa kwa ajili ya kusafirishia abiria majini  Katika Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.Picha na Kenneth Ngelesi

Na EmanuelMadafa,Mbeya
MAMLAKA ya udhibiti na usafiri wa nchi kavu na majini (SUMATRA) inatarajia kubadilisha matumizi ya mitimbwi ya kienyeji inayo tumika kusafirisha abiria kwenye bahari, maziwa na mito kutokana na vyombo hivyo kukosa ubora na umathubuti hali inayohatarisha usalama wa watu, vyombo na mali.

Akizungumza na Blogu hii   kwenye maonyesho ya Sherehe za NaneNane Nyanda za Juu Kusini yanayoendelea katika  viwanja vya John Mwakangale vilivyopo eneo la Uyole Jijini Mbeya,Ofisa Udhibiti wa Majini, Adam Mamilo, amesema mitumbwi mingi imejengwa kwa kienyeji tena kwa kutumia mbao ambazo si elekezi.

Alisema, mitumbwi hiyo hutengenezwa kwa kutumia mbao ambazo hazikidhi viwango hali inayochangia kupoteza uhai wake ambao upo kwenye wastani wa miaka 3 hadi 5 ukilinganisha na miaka 35 kwa vyombo vilivyojengwa kwa viwango.

Amesema, kinachojitokeza katika hali hiyo,ni kupungua kwa ubora na umathubuti wa vyombo hivyo vinavyoundwa na kuhatarisha usalama wa watu, vyombo na mali.

Amesema, utafiti huo ulibaini kuwa miundo na uundaji wa boti au mitumbwi inayotumika Tanzania ni ule wa kutumia miti mikubwa na kuchimba umbile la chombo na unatumika kwa vyombo vidogo kwenye baharini, maziwa na mtoni.

Amesema kuwa mitumbiwi hiyo si salama  kwa matumizi ya binadamu kwani hutengenezwa kwa kutumia miti mikubwa ambayo huchimbwa umbile la chombo na kutumika kwa vyombo vidogo baharini, mtoni na maziwa jambo ambalo limekuwa hatari zaidi mara mawimbi yanapopiga kitendo ambacho kinahatarisha uhai wa mtumiaji.

.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages