LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jul 31, 2014

LAFARGE YAIPIGA JEKI CHUNYA TANI 50 ZA CEMENT KWA AJILI YA UJENZI WA UWANJA


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Ndugu Deodatus Kinawilo wa Kwanza kushoto akipokea msaada wa cement toka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Lafarge Ndugu Catherine Langreney wa Pili kulia kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa michezo uliopo eneo la Kiwanja Wilayani Chunya Mkoani Mbeya.

Mkurugenzi Mtendaji Mtendaji wa Kampuni ya Lafarge Ndugu Catherine Langreney akizungumza katika makabidhiano hayo katika eneo la mradi.
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Ndugu Deodatus Kinawilo akizungumza mara baada ya kupokea msaada wa Cement mifuko 1000 ambayo ni sawa na Tani hamsini  toka kwa kampuni ya Lafarge amabo wanazalisha cement ya Tembo.
Katibu wa ujenzi wa uwanja huo wa michezo Ndugu Solo Tuyajage akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo
Mkuu wa Wilaya hiyo akitoa ufafanuzi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Lafarge namna uwanja huo utakavyo kuwa



PICHA NA JAMIIMOJA

Na EmanuelMadafa,mbeya
Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya amepokea msaada wa Tani hamsini za Cement kutoka kiwanda cha Mbeya Cement (Lafarge) kwa lengo kupiga jeki  ujenzi  wa kisasa wa michezo utakaogharimu jumla ya sh. Bilioni 8.

Aidha uwanja huo utakuwa na  uwezo wa kuchukua watazamaji 50,000 pia unatarajiwa kuwa kitega uchumi cha aina yake kuwepo katika wilaya ya Chunya na mkoa wa Mbeya kwa ujumla.

Akizungumza katika makabidhiano ya msaada huo Mkurugenzi Mtendaji  wa Kampuni ya Lafarge Ndugu Catherine Langreney amesema kuwa kampuni yake imepokea maombi hayo kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya na kukubali kuchangia saruji mifuko 1000 ambayo ni swan a Tani 50 .
Langreney amesema wamepata msukumo mkubwa wa kuchangia mifuko hiyo kutokana na Halmashauri hiyo kupanua wigo wa ajira hasa kutokana hatua yake ya kuanzisha kwa mpango wa ujenzi wa uwanja huo.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo amesema kuwa msaada huo utafungua mahusiano mapya kati ya kampuni yake na serikali ya wilaya ya Chunya katika Nyanja mbalimbali za kimaendeleo.

Aidha amesema kuwa  mbali na kufanya biashara kampuni yake inachangia huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi waliopo maeneo ya karibu na kiwanda chao hivyo msaada huo ni sehemu ya huduma zao za kawaida kwa wananchi.
Hata hivyo Ndugu Langreney ameweka bayana kuwa kampuni yake itahakikisha inashirikiana na Halmashauri hiyo  katika ujenzi bora wa makazi ya watu kwa kutoa teknologia mpya ya kujenga miji bora kwa hgarama nfuu.
Akipokea msaada huo Mkuu wa Wilaya ya Chunya  Deodatus Kinawiro amesema kuwa uwanja huo unajengwa na wananchi wenyewe kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya hiyo ambapo pendekezo la ujenzi wa uwanja huo aliliwasilisha kwenye vikao vya halmashauri na kuridhiwa na baraza la Madiwani.

Amesema teyari  Halmashauri ya wilaya ya Chunya imepitisha azimio la kuchangia   Sh. Milioni 70 katika bajeti yake ambapo feza hiyo itatolewa kwa amwamu tofauti  ambapo kila mwananchi  kuchangia  sh.2000 kwa kwa kipindi cha miaka mitatu hadi 2016 ambapo uwanja huo utakuwa umekamilika .
Amesema endapo uwanja huo utakamilika kwa wakati kama ilivyo pangwa uzinduzi wake utambatana na miaka 75 ya kuanzishwa kwa Halmasahuri hiyo ambapo sherehe hizo kufanyika ndani ya uwanja huo.

Pia mkuu huyo wa Wilaya ametoa pongezi zake kwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo kwa hatua yake ya kuchangia mifuko hiyo 1000 huku akiendelea kutoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kuchangia ujenzi wa uwanja huo.


Naye  Katibu wa Kamati ya Ujenzi wa uwanja huo Solo Tuyagaje amesema kuwa hadi sasa jumla ya sh. Milioni 107 zilichangwa na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na makampuni yanayochimba madini wilayani humo na wachimbaji wadogo.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages