LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 4, 2017

KINANA ATEMBELEA KIJIJI CHA MATUMAINI, ASHUHUDIA KINAVYOJITOLEA KUSAIDIA JAMII HASA KULEA WATOTO YATIMA, MKOANI DODOMA LEO

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwakabidhi msaada wa vyakula watoto wa Kijiji cha Matumaini, kilichopo eneo la Kisasa Dodoma mjini alipotembelea kituo hicho kuwafariji watoto yatima, leo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM, ambayo kilele chake ni kesho. Kushoto ni mwanzilishi wa Kijiji hicho Padre Vincent Boseil
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na watoto wanaolelewa katika Kijiji cha Matumaini, kilichopo eneo la Kisasa Dodoma mjini alipotembelea kituo hicho kuwafariji watoto yatima, leo ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 40 ya CCM, ambayo kilele chake ni kesho. Kulia ni mmoja wa waanzilishi wa kituo hicho Sista Roselie
 Kinana akikaribishwa ndani na Mwanzilishi wa Kituo hicho, Padre  Vincent Boseili
 Kinana akisaini kitabu cha wageni alipowasili kwenye kituo hicho cha Kijiji cha Matumaini
 Padre Vincenti akionyesha wageni ramani ya Kijiji hicho cha Matumaini
 Sista Roselie akisoma risala
 Padre Vincent akitoa maelezo kuhusu kijiji hicho cha Matumaini
 Waziri Mavunde akizungumza alipokaribisha kuongea kwenye kijiji hicho cha Matumaini
 Mavunde akizungumza


Mavunde akipongezwa na Kinana baada ya kuzungumza neno la shukrani kwa mwanzilishi wa Kijiji hicho chenye kituo cha watoto yatima
Kinana akimpongeza Padre Vincent baada ya kuzungumza maneno ya shukrani
Kinana na ugeni wake wakienda kukagua sguhuli mbalimbali kwenye Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akiwasalimia watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho ambao pia wanasoma
Kinana akiwasalimia wanafunzi wa Sekondari wanalelewa na kusomeshwa na Kijiji hicho cha Matumaini. Kushoto ni Padre Vincent wa Kijiji hicho
Watoto ambao ni wanafunzi wanaolelewa na kusomeshwa kwenye Kijiji hicho wakiimba wimbo wa Taifa Kinana alipowasili
Wanafunzi wa Kijiji hicho wakipiga ala wakati wimbo wa Taifa la Tanzania ukiimbwa
Kinana akifurahia jambo kwa kupiga kofi huku mtoto wa Kijiji hicho aliyempakata naye akipiga kofi
Wanafunzi wa Sekondari wanaolelewa na kusomeshwa na Kijiji hicho cha Matumaini wakiimba wimbo wao maalum
Kinana akiwafurahia wanafunzi ambao alitambulishwa kwao na Padre Vincent
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimfurahia mtoto anayelelewa katika Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akikabidhi zawadi kwa watoto
Kinana akifurahia watoto wa Kijiji hicho baada ya kuwapa zawadi
Kinana akishiriki kuimba wimbo maalum pamoja na wanafunzi wanaolelewa na kusomeshwa katika Kijiji hicho
Kinana akionyeshwa eneo ambako kinamama hujifungulia bure kwenye Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akizungumzana wageni kutoka Italia ambao nao walifika kutembelea Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akionyeshwa eneo ambako hutunza watoto wachanga, ambao ni yatima, kwenye Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akimchukua mtoto mmoja kumfurahia, katika eneo hilo la kulea watoto wachanga
Kisha Kinana akamchumu mtoto huyo kwa upendo mkubwa
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Christina Mndeme, akimchukua mtoto kwa upendo
Watoto katika Kijiji hicho wakitazama kwa mshangao ugeni wa Kinana 
Katibu Mkuu Kinana akipewa maelezo kwenye mapokezi ya Hospitali ya Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akionyeshwa vifaa vya kupimia CD4 kwa wagonjwa wa Ukimwi
Kinana akimshukuru Padre Vincent baada ya kutembelea Kijiji hicho cha Matumaini
Kinana akiagana na Padre Vincnt kabla ya kuondoka. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme
Mkuu wa wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme akiagana na Padre Vince pia kabla ya kuondoka. Picha zaidi/BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages