LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 4, 2017

KINANA ASHIRIKI NA KAGUA SHUGHULI ZA MAENDELEO DODOMA MJINI IKIWA NI SEHEMU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 40 YA CCM AMBAYO KILELE CCHAKE NI KESHO

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Wilaya ya Dodoma mjini na mkoa huo, katika Ofisi ya CCM mkoa wa Dodoma, leo alipowasili kwenye ofisi hiyo, tayari kushiriki na kukagua shughuli za maendeleo ikiwa ni sehemu ya Madhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho. Akizungumza Kinana amesema, CCM imeamua kufanya Maadhimisho hayo mkoani Dodoma kwa kuwa imedhamiriwa kuisaidia Serikali katika kutekeleza ilani ya CCM, hivyo CCM imeamua kufanya hivyo ili kuunga mkono azma ya Serikali kuhamia Dodoma.
 Mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana akitoa salamu za shukrani, baada ya Kinana kuzungumza katika mkutano huo wa ndani. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa huo, Adam Kimbisa.
 Katibu  Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akiwasalimia mafundi alipowasili kukagua na kupanda miti kwenye mradi wa Ujenzi wa Dampo la Kisasa katika eneo la Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini, leo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho.
 Katibu  Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akipanda miti kwenye mradi wa Ujenzi wa Dampo la Kisasa katika eneo la Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini, leo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya CCM ambayo kilele chake ni kesho.
 Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Dodoma Mjini, akishiriki kupanda mji kwenye mradi huo
 Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Christina Mndeme akishiriki kupanda mti kwenye eneo la mradi huo
 Mbunge wa Dodoma Mjini, Waziri Anthony Mavunde akishiriki kupanda mti katika eneo hilo
 Kinana akimpongeza kwa kupanda mti katika eneo hilo, Mzee Godfrey James
 Kinana akimsaidia kupanda mti mjumbe wa shina katika kata hiyo Ester Paschal
 Kinana na ujumbe wake wakiondoka katika upandaji mti na kwenda kukagua ujenzi wa dampo la kisasa katika eneo hilo. Kushoto ni Mavunde na kulia ni Kimbisa
 Mhandisi wa Manispaa ya Dodoma, Injinia John Nchilla akimpa Kinana maelezo kuhusu ujenzi wa dampo hilo la Kisasa katika Kata ya Matumbulu wilaya ya Dodoma Mjini
 Mwenyekiti wa CCM, Kata ya Nkuhungu, Dodoma Mjini, Pius Afa akimkaribisha Kinana kushiriki ujnezi na kupanda mti kwenye ujenzi wa Ofisi ya CCM ya Kata hiyo
 Wanachi wakimpokea Kinana kwa shamrashamra alipowasili katika Kata hiyo ya Nkuhungu
 Kinana akisalimia wananchi wa Nkuhungu
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Nkuhungu Pius Afa akimuonyesha Kinana ramani ya ujenzi wa Ofisi hiyo ya CCM ya Kata hiyo
 Kinana akipokea tofali alipokuwa akishiriki ujenzi wa Ofisi hiyo ya CCM Kata ya Nkuhungu
 Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Nkuhungu, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40ya CCM ambayo kilele chake ni kesho
 Kinana akishuka baada ya kushiriki ujenzi wa Ofisi hiyo kikamilifu
Kinana akizungumza na wananchi baada ya kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Mkuhungu, Dodoma leo. Picha zaidi  alipotembelea Kijiji cha Matumaini/BOFYA HAPA

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages