LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Sep 16, 2016

MHE PINDI CHANA AHUDHURIA MKUTANO WA AU KUHUSU HAKI ZA WAPIGAKURA

Mhe Pindi Chana wa kwanza kulia akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa Umoja wa Afrika kuhusu haki za Wapigakura, unaofanyika Addis Ababa, Ethiopia

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Siasa na Uhusiano ya Kimataifa (SUKI) Dkt Pindi Chana amehudhuria mkutano wa Umoja wa Nchi za Afrika (AU) unaofanyika katika ukumbi wa AU mjini Addis Ababa, Ethiopia

Mkutano huo ambao umehusisha viongozi na wawakilishi wa vyama vya siasa, mashirika na taasisi za kidini na kimila pamoja na wadau mbalimbali wa demokrasia na haki za Wananchi umejadili kuhusu namna bora ya kutunza na kutetea haki za wapigakura barani Afrika.

Dr Pindi Chana amekiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano huo muhimu wa siku nne unaotarajia kumalizika tarehe 18 Septemba, 2016.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa SUKI, Dkt Pindi Chana akiwa na Ndg Nana Agyakoma,(Mother of Mampong) Kiongozi wa Kimila kutoka nchini Ghana ambae amehudhuria mkutano wa Umoja wa Afrika kuhusu haki za wananchi.

Dkt Pindi Chana akiwa kwenye mkutano wa Umoja wa Africa (AU) kuhusu haki za wananchi uliohudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Taasisi za Kimila na Kidini, vyama vya siasa na wadau wa demookrasia na haki za wapiga kura.


No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages