LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 8, 2015

NAPE AKABIDHI PIKIPIKI 20 KWA MAKATIBU KATA JIMBONI KWAKE


 Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akimkabidhi Katibu wa kata ya Mtua Kilimahewa Ndugu Maliki funguo ya pikipiki kwa niaba ya makatibu kata 20 wa jimbo hilo ambao wote wamewezeshwa usafiri wa pikipiki ili kurahisisha ufanisi wa kazi zao.
 Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye akijaribu moja ya pikipiki kati ya 20 alizowapa makatibu kata ili ziweze kuwasaidia kufanya kazi kwa ufanisi kwenye shughuli zao za kujenga na kuimarisha Chama Cha Mapinduzi.
 Sehemu ya pikipiki zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye kwa makatibu kata 20 wa jimbo hilo.
Mbunge wa Jimbo la Mtama Ndugu Nape Nnauye akizungumza mbele ya viongozi wa CCM wilaya ya Lindi vijijini ambapo aliwaambia viongozi hao kuwa amejipanga kufanya kazi katika jimbo hilo zenye kuleta tija na kuhakikisha anatekeleza ahadi zote alizozitoa wakati wa kampeni na kuwata makatibu kata waliokabidhiwa pikipiki 20 kuzitumia katika kazi za kujenga na kuimarisha chama.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages