LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Nov 15, 2015

JK AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU MJINI DODOMA

 Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ambapo ajenda kuu ilikuwa kujadili majina ya wana-CCM walioomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Uspika na Unaibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philipo Mangula na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kulia).
 Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM kikiendelea ndani ya ukumbi wa NEC, Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi mjini Dodoma.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Peramiho Mhe. Jenista Muhagama muda mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha kamati kuu mjini Dodoma.
Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro akizungumza na Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Mhe. Zakhia Meghji muda mfupi kabla ya kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ambayo ilikuwa na ajenda ya kujadili majina ya wana CCM walioomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Spika na Unaibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages