LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Apr 7, 2016

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI SHUGHULI ZA KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA KIMBARI (KWIBUKA) KIGALI NCHINI RWANDA



Na Mwandishi Maalumu, RWANDA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli wameungana na wananchi wa Rwanda kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 22 ya tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari yaliyosababisha vifo vya watu takribani milioni 1.

Maadhimisho hayo yamefanyika katika eneo la Gisozi Mjini Kigali, yalipo makumbusho ya mauaji ya Kimbari ambapo Rais Magufuli na Mkewe wakiwa na mwenyeji wao Rais Paul Kagame wa Rwanda na Mkewe Mama Janeth Kagame wameweka shada la mauaji katika eneo walipouawa idadi kubwa ya wananchi wa Rwanda na pia wakawasha mwenge wa matumaini kwa walionusurika katika mauaji hayo na kwa Taifa zima la Rwanda.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakisali mbele ya makaburi ya watu waliouwawa katika Mauaji ya Kimbari nchini Rwanda mwaka 1994. Kulia ni Rais wa Rwanda Paul Kagame pamoja na Mkewe Janeth Kagame na mtoto.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame wakiwasha mwenge wa matumaini kuashiria kutotokea tena kwa mauaji ya Kimbari nchini Rwanda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame, mama Janeth Magufuli, Mama Janeth Kagame wakisikiliza historia ya jinsi mauaji ya kimbari yalivyotokea katika eneo la kumbukumbu ya mauji hayo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame, mama Janeth Magufuli, Mama Janeth Kagame wakiwa wamesimama kutoa heshima kwa watu waliofariki katika mauaji hayo ya kimbari.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiangalia kwa uchungu mafuvu ya watu waliopoteza maisha katika mauaji hayo ya kimbari.
............................................................
Pamoja na kupata historia ya mauaji hayo ya kimbari, Rais Magufuli akiongozwa na mwenyeji wake Rais Kagame ametembelea jumba maalum lililohifadhi kumbukumbu ya watu waliopoteza maisha, ambapo amepata maelezo kutoka kwa wahifadhi wa makumbusho hiyo, na pia kujioonea picha na mabaki ya mifupa na mafuvu ya binadamu waliouawa.

Akizungumza mara baada ya kutembelea jumba hilo la makumbusho Rais Magufuli ameelezea kusikitishwa kwake na mauaji hayo na kusema tukio hilo halipaswi kurudia.

"Haitatokea tena, hatuwezi kubadilisha yaliyopita lakini tunaweza kubadilisha mambo ya sasa na yajayo, mauaji haya hayapaswi kutokea tena" Amesema Rais Magufuli. 

Wageni mbalimbali waliofika kwenye kumbukumbu hizo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia picha za watoto waliouwawa kinyama katika eneo la Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbari  Gishozi Kigali nchini Rwanda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini Kitabu katika Jengo la makumbusho ya mauaji ya Kimbari Gishozi Kigali nchini Rwanda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea kitabu chenye maelezo mbalimbali kuhusu mauaji hayo ya kimbari.
Rais wa Rwanda Paul Kagame akimpokea Rais Magufuli katika viwanja vya Gishozi kabla ya kwenda kuweka mashada ya maua kwenye makaburi ya watu waliouwawa katika mauaji ya Kimbari.
Rais wa Rwanda Paul Kagame akiwa na Rais Magufuli pamoja na Mama Janeth Magufuli, Janeth Kagame wakielekea kwenye makaburi ya halaiki katika makumbusho ya mauaji ya Kimbari, Gishozi Kigali nchini Rwanda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakisali mbele ya makaburi ya watu waliouwawa katika Mauaji ya Kimbari nchini Rwanda mwaka 1994. 

Rais Magufuli ambaye aliingia nchini Rwanda jana tarehe 06 April, 2016 ikiwa ni ziara yake ya kwanza nje ya nchi tangu aingie Madarakani Tarehe 05 Novemba, 2015 ameondoka Mjini Kigali jioni hii na kurejea Jijini Dar es salaam.


PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages