LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Feb 20, 2016

DKT.KIGWANGALLA AFANYA KIKAO CHA PILI NA KIKOSI KAZI CHA KUBORESHA HUDUMA ZA MFUKO WA AFYA YA JAMII (CHF)


kamati 2 kigwangalla
Baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi hicho wakiendelea na majumu yao.
Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla amekutana kwa mara ya pili na kikosi kazi cha watu 24 ambacho kitakuwa na kazi ya kutengeneza mpango mkakati wa kuwezesha kuboresha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Mkutano unaoendelea katika ukumbi wa Wizara hiyo ya Afya, leo Februari 20th, 2016 unachambua mambo mbalimbali ya kuweza kuyafanyia maboresho na ya kimkakati ilikuweza kufikia malengo ya Mfuko huo wa Afya ya Jamii (CHF).
Katika Mkutano huo, Dkt. Kigwangalla ni mwenyekiti wa kikosi kazi hicho ambapo kwa ujumla na wajumbe hao wapo kupanga mikakati thabiti.
Baadhi ya Wajumbe wa kikosi kazi hicho wanaoshiriki kikao ni pamoja na Prof. Angwara Kiwara, Prof. Phares Mujinja, Dkt. Francis Frederick, Dkt. Heri Marwa, Dkt. Deogratius Pisa, Dkt. Amos Kahwa, Irene Kiria, Semkae Kilonzo, Gemini Mtei, Dkt. Jehovaness Aikaeli na Obey Assey.
Wengine ni Mathias Kabunduguru, Dkt. Dereck Chitama, Prof. Flora Kessy, Florence Mwanri, Athuman Rehani, Maximillian Mapunda, Bedason Shallanda, Daniel Ngowi, Beng' Issa, Edwin Mikongoti, Hussein Sengu, Dkt. Beatus Leon na Dkt. Pastory Sekule.
imeandaliwa na Andrew Chale,modewjiblog
kamat66
Mkutano huo ukiendelea.
kamati 78Baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi hicho wakimsikiliza Naibu Waaziri wa Afya Dkt.Kigwangalla (Hayupo pichani) wakati wa mkutano huo unaoendelea Wizarani hapo.
kamati 8
kamatii
kamati 3
Naibu Waziri Dkt.Kigwangalla ambaye ni Mwenyekiti wa kikosi kazi hicho (kulia) akiwa pamoja na baadhi ya wajumbe hao. (Picha zote na Andrew Chale,modewjiblog).

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages