LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Jan 1, 2016

MKESHA WA KULIOMBEA TAIFA NA VIONGOZI WAKE WAFANA JIJINI DAR ES SALAAM

 Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Wiliam Lukuvi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, akihutubia kwenye Mkesha Mkubwa Kitaifa,Dua Maalum ya kuwaombea viongozi na Taifa uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
 Mchungaji Eden Godfrey akihubiri kwenye Mkesha Mkubwa Kitaifa, Dua maalum uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.

 Viongozi wakiwa wameshikana mikono wakati wa maombi maalum kwa Taifa na Viongozi wake .
 Umati wa wakazi wa jiji la Dar es salaam waliojitokeza kwenye ibada maalum ya mkesha wa mwaka mpya uliofanyika kwenye uwanja wa Uhuru.
 Wananchi wakiwa kwenye maombi ya kuliombea Taifa Amani, na kuwaombea viongozi wake afya njema.
 Mwalimu Teddy Kwilasa akitoa maombi maalum kwa Taifa kwenye mkesha wa mwaka mpya.
 Wananchi wakiwa kwenye maombi mazito ya kuwaombea Viongozi wa Taifa letu
 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi (wa pili kulia) akiwa pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye pamoja na wake zao wakiupokea mwaka kwenye Mkesha Mkubwa Kitaifa, ambapo Taifa na Viongozi wake waliombewa.
 Sehemu ya Vijana waliojitokeza kwenye mkesha mkubwa uliofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akitoa salaam maalum za kuwataka wazazi kuwafundisha watoto wao umuhimu wa amani ya nchi wakati wa mkesha wa mkubwa kitaifa wa kuombea Taifa na Viongozi wake dua maalum.
 Bi. Christina Elias wa Aleluyah kwaya kutoka Tabata  akiimba kwa hisia kwenye mkesha mkubwa wa kitaifa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
 Viongozi wakiwa kwenye maombi maalum ambapo waliwakilisha Mawaziri wote nchini.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages