LATEST HEADLINES👉

Your Ad Spot

Dec 4, 2015

MBUNGE WA JIMBO LA FUONI ZANZIBAR MHE. ABAAS MWINYI


Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe A bass Ali Hassan Mwinyi, akitembelea Kituo cha Afya cha Fuoni Zanzibar kinachotowa huduma kwa Wananchi wa Jimbo hilo na jirani wakati akitimiza ahadi yake kwa kutuo hicha, akipata maelezo kutokwa kwa mdhamini wa kituo hicho Muuguzi wa Afya ya Jamii Bi Mwaka Pandu Makame akitowa maelezo ya eneo lao la kuchomea taka za kituo hicho.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassan Mwinyi akitembelea kituo hicho cha Afya Fuoni Zanzibar akiwa katika ziara yake katika jimbo lake kujiuonea ufanisi wa kituo hicho na kukabidha Madawa na kuvifanyia mategenezo vyoo vya kituo hicho ni moja ya kero za Wananchi wanaofika kituoni hapo. 
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Adass Mwinyi akitembezwa katika kituo hicho na Madaktari wa Kituo hicho, akiwa katika ziara yake ya kukamilisha ahadi yake juu ya kituo hicha kikifanyia mategenezo sehemu. 
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Mwinyi akimsikiliza daktari wa kitengo cha kungolea meno katika Kituo hicho cha Fuoni Zainab Seif na Khadija Khamis, wakimueleza Mbunge huyo baadhi ya vifaa vinakosekana katika kitengo chao kwa ajili ya huduma ya kungolea meno Wananchi wanaofika kituoni hapo. Kituo hicho kinatowa huduma za Uzalishaji wa Kinamama kupiga Utra saund na huduma nyengine za matibabu 
Mbunge wa Fuoni Mhe Abass Mwinyi akizungumza wa Wafanyakazi wa Kitengo cha Meno katika Kituo cha Afya Fuoni wakati wa ziara yake kutimia ahadi alizotowa kwa Wananchi wa Jimbo hilo katika kituo hicho na kufanikisha upatikanaji wa vifaa hivyo wanavohitaji katika kituo hicho kuondoa kero kwa Wananchi wake wanaofika kituoni hapo kupata huduma ya meno na nyeginezo.
Mhe Abass Mwinyi akizungumza na Wafanyakazi wa Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar wakati wa ziara yake kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa kwa ajili ya kituo hicho, Kinachotowa huduma kwa Wananchi wa Jimbo lake na Wananchi wa jirani.ili kuboresha ufanisi wa huduma ya Afya kituoni hapo.    
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe. Abass Mwinyi akizungumza na wafanyakazi wa Kituo hicho na Wananchi wa Jimbo lake wakati wa ziara yake ya kwanza katika jimbo hilo na kukabidhi vifaa na Madawa kwa kituo hicho. Mhe Mbunge Abass amesema sasa Hapa Kazi Tu, ili kuwaletea maendeleo Wananchi wa Jimbo lake na kuondoa kero zote katika jimbo hilo na kuwa Jimbo la mfano katika majimbo yote ya Zanzibar. 
Daktari Dhamana wa Kituo cha Afya Fuoni Said Fadhili Abass akizungumza wakati wa mkutano huo na Mbunge wa Jimbo la fuoni na kumshukuru kwa msaada wake huo kwa Kituo chao. na kusema dawa hizo zitatumika kwa wananchi wa Jimbo hilo wanaofika kituoni hapa kupata huduma mbalimbali za Afya.  
Wauguzi wa Kituo cha Afya Fuoni wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe Abass Mwinyi wakati akizungumza na Wafanyakazi hao katika ziara yake kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa kwa ajili ya Wananchi wanaofika kupata huduma kituoni hapo.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi fedha shilingi milioni moja Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar Said Fadhil Abass, kwa ajili ya kutatua makero zinazokikabili kituo hicho cha Afya Fuoni ili kufanya kazi zao kwa kuwahudumia Wananchi kwa ufanisi zaidi.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi madawa Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar Said Fadhil Abass, kwa ajili ya matumizi ya kituo hicho kinachotowa huduma mbalimbali kwa Wananchi wa Fuoni zikiwemo za kuzalisha kinamama na upigaji wa vipimo vya utra sound katika kituo hicho na kulaza wagonjwa. 
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Ali Hassaan Mwinyi akimkabidhi vifaa kwa akili ya vyoo vya kituo hicho Dakt. Dhamani wa Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar Said Fadhil Abass na kulia Muuguzi wa Afya ya Jamii Kituoni hapo Mwaka Pandu Makame. 
Mzee wa Jimbo la Fuoni Mzee Takrima akizungumza wakati wa hafla hiyo ya kukabidhi madawa na vifaa katika Kituo cha Afya Fuoni Zanzibar.
Wananchi wa Jimbo la Fuoni wakimsikiliza Mbunge wao. 
Wauguzi wa Kituo cha Afya Fuoni wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe Abass Mwinyi wakati akizungumza na Wafanyakazi hao katika ziara yake kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa kwa ajili ya Wananchi wanaofika kupata huduma kituoni hapo.
Mwananchi wa Jimbo la Fuoni akitowa shukrani na kumtaka Mbunge wa Jimbo hilo kukabidhiwa gari ya wagonjwa kwa ajili ya kuihudumia kutowa huduma kwa Wananchi wanaofika kituoni hapo kupata huduma gari hiyi hutumika kwa Wananchi kesi zao zinapokuwa zimeshindikana hapo na kuhamishiwa katika Hospitali ya Rafuu ya Mnazi Mmoja Zanzibar. 
Sheha wa Shehia ya Pangawe Jimbo la Fuoni akitowa shukrani kwa Mhe Mbunge Abass Mwinyi kwa msaada wake katika Kituo chao na kumtaka Mbunge huyo kufutalia ajira za Vijana wanaojitolea katika Kituo hicho sasa karibu miaka miwili hufanya kazi ya kuwahudumia wagonjwa wanaofika kituo hapo bila ya kuajiriwa amemuomba mbunge huyo kufuatilia swala hilo.
Wauguzi wa Kituo cha Afya Fuoni na Wananchi wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe Abass Mwinyi wakati akizungumza na Wafanyakazi hao katika ziara yake kutembelea Kituo hicho na kukabidhi madawa kwa ajili ya Wananchi wanaofika kupata huduma kituoni hapo.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Mhe Abass Mwinyi akiitikia dua baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya kukabidhi vifaa katika kituo cha afya fuoni Zanzibar.
  Wananchi na Waguzi wa kituo hicho wakiitikia dua baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya kukabidhi vifaa.
Mbunge wa Jimbo la Fuoni Zanzibar Mhe Abass Mwinyi akiwa na Wauguzi wa kituo hicho wakibadilisha mawazo baada ya hfla hiyo akiwa katika eneo la kituo hicho fuoni Zanzibar.
Imetayarishwa na othmanmapara.Blogspot 
Zanzinews.com
Email othmanmaulid@gmail.com.
Mobile 0777424152 or 0715424152.

No comments:

Post a Comment

ANDIKA MAONI (COMMENTS) HAPO👇

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages